Posts

Showing posts from June 21, 2012

RAIS KIKWETE ATEMBELEA SHAMBA LA MFANO LA KIJIJI CHA KICHOPELO,BAHI,MKOANI DODOMA

Image
Rais Dkt .Jakaya Mrisho Kikwete akikagua   nyanya   na mazo mengine ya mboga pamoja na mizabibu katika shamba linalomilikiwa na kampuni ya kilimo ya Tendaji Trade huko katika kijiji cha Chikopelo,wilaya ya Bahi, Mkoani Dodoma   leo asubuhi.Kushoto ni mmoja wa wamiliki wa Shamba hilo Bwana Alon Hoven anayeshirikiana na Bwana Dunstan Mrutu(hayupo pichani).shamba hilo linamwagiliwa kwa kutumia teknolojia ya   matone(Drip irrigation system). Mmoja wa Wamiliki wa Shamba la Mboga katika kijiji cha Chikopelo Bwana Alon Hoven kimwonesha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete baadhi ya mazao yanayozalishwa kwa kutumia mbegu bora pamoja na teknolojia ya ya umwagiliaji wa matone wakati Rais alipotembelea shamba hilo katika kijiji cha Chikopelo, wilayani Bahi,mkoani   Dodoma leo asubuhi.Shamba hilo lenye ukubwa wa hekari mia moja linamilikiwa na kampuni ya kilimo ya Tendaji Trade chini ya Bwana Dunstan Mrutu na Alon Hoven raia wa Israel. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Rais Kikwete ali
Image
Mkutano Mkuu wa Dharura wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) utafanyika Juni 23 mwaka huu kwenye ukumbi wa Msimbazi Centre, Dar es Salaam kuanzia saa 2.00 asubuhi.             Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa TWFA, Lina Kessy, ajenda kuu katika mkutano huo ni marekebisho ya Katiba ya chama hicho yanayotokana na maelekezo ya Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) juu ya marekebisho kwenye katiba za wanachama wake ambazo zina upungufu. Tayari mapendekezo ya marekebisho hayo kulingana na mwongozo wa TFF yalishapitiwa na Kamati ya Utendaji ya TWFA. Mbali ya Kamati ya Utendaji, wajumbe wengine wa mkutano huo ni Mwenyekiti, Katibu na mjumbe wa Mkutano Mkuu kutokana vyama vya mpira wa miguu wa wanawake vya mikoa ya Tanzania Bara. Wajumbe watafikia kwenye hosteli ya Msimbazi Centre ambapo wanatakiwa kuripoti siku moja kabla ya mkutano huo. Mgeni rasmi atakayefungua mkutano

MATOKEO YA PICHA BUNGENI

Image
  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda (kulia) akibadilishana mawazo na Mbunge wa Kuteuliwa Anna Abdallah (kushoto) leo mjini Dodoma katika viwanja vya Bunge.   Picha na Tiganya Vincent-Dodoma Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa     TAMISEMI , Aggrey Mwanri jana mjini Dodoma katika viwanja vya Bunge.

Arsenal tayari kununua hisa zaidi

Image
Alisher Usmanov Tajiri mmoja anayemiliki kiasi kikubwa katika hisa za klabu ya Arsenal, Alisher Usmanov anasema angependa kununua hisa zaidi za klabu hio ingawa hana nia ya kupata nafasi kwenye bodi inayoongoza klabu. Usmanov ambaye ndiye tajiri mwenye vipesa kuliko tajiri mwingine nchini jimbo la zamani la Urussi la Uzbekistan, ni mmoja wa matajiri kadhaa wanaomiliki hisa katika klabu za Uingereza kama Roman Abramovich huko Chelsea na Anton Zingarevich wa Reading. Arsenal fc Usmanov ameliambia shirika la habari la Reuters nje ya mji wa Petersburg kua 'daima na kwa kiwango chochote, nipo tayari kuongezea kiwango cha hisa zangu. Usmanov, ambaye utajiri wake umetokana na biashara ya chuma na teknolojia anaweza kujijengea umaarufu na nafasi kwenye b

Zaidi ya watu 50 wafariki dunia kwenye ajali ya boti nchini Malawi

Image
  Habari kutoka Malawi zinasema kuwa zaidi ya watu 50 wamefariki dunia kwenye ajali ya boti iliyotokea katika ziwa Malawi. Maafisa wa polisi wa nchi hiyo wamesema kuwa boti hiyo ilikuwa na wahajiri haramu kutoka Somalia na Ethiopia ambao lengo lao lilikuwa ni kufika Malawi na kisha kuingia kinyemela Afrika Kusini. Baadhi ya duru zinaarifu kuwa Watanzania kadhaa pia ni miongoni mwa waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo. Imedaiwa kwamba boti hiyo ilizama siku ya Jumanne na miili kuanza kuelea siku iliyofuatia. Maafisa wa usalama wamesema kuwa tayari miili 47 imeopolewa na kuzikwa kwenye kaburi la pamoja. Ripoti ya hivi majuzi ya shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch imesema visa vya magendo ya binadamu barani Afrika vimezidi mno katika miezi minne ya kwanza ya mwaka huu wa 2012 ikilinganishwa na miezi minne ya kwanza ya mwaka uliopita.

DIDIER DROGBA AHAMIA CHINA

Image
Aliyekuwa mshmabulizi matata wa Chelsea Didier Drogba amehamia klabu ya Shanghai Shenhua ya China. Didier Drogba sasa ahamia klabu ya China Mwamba huyo ametia kandarasi ya miaka miwili-na-nusu na timu hiyo ya China. Kujiunga na klabu hicho , kimemfanya awe timu moja na mchezaji mwengine wa Chelsea Nicolas Anelka. Drogba mwenye umri wa miaka 34 amesema kabla ya kuamua kuhamia China alifikiria kwa makin sanai. "Nilitilia maanani mialiko chungu nzima niliopata katika kipindi cha wiki chache zilizopita , lakini nafikiri kwa wakati huu kuhamia timu ya Shanghai Shenhua ulikuwa uamuzi mzuri" Mwamba huyo wa Ivory Coast atakumbukwa kwa bao alilofungia Chalsea walipocheza na Bayern Munich ya Ujerumani.Bao hilo liliifanya Chalsea ijiandikie historia ya kushinda kombe la Klabu bingwa bara Ulaya.

LEO NI SIKU YA IBADA

Image
    Leo ni Alkhamisi tarehe Mosi Shaaban mwaka 1433 Hijria sawa na tarehe 21 J uni 2012 Miladia. Mwezi wa shaabani unaoanza leo ni mwezi wa ibada, kujipinda na kuomba maghufira. Mtume Muhammad (saw) aliutukuza mno mwezi huu na kuuita kuwa ni Mwezi wa Mwenyezi Mungu SW. Mtume na maimamu watoharifu katika kizazi chake waliusia mno kufanya ibada hususan kufunga swaumu katika mwezi huu wa Shaabani kwa sababu ndio unaotayarisha uwanja mzuri wa kuingia kwenye mwezi wa ugeni wa Mwenyezi Mungu na wenye baraka tele wa Ramadhan. Katika mwezi huu wa Shaabani kumetukia mambo mengi muhimu kama kuzaliwa Imam Hussein bin Ali (as) mjukuu wa Bwana wetu Muhammad (saw) na pia tukio la kuzaliwa Imam wa Zama Mahdi (as) Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake. Tarehe Mosi Shaabani miaka 167 iliyopita alifariki dunia mwanazuoni mkubwa wa Kiislamu Sheikh Muhammad Hassan Najafi maarufu kwa lakabu ya Sahib al Jawahir. Sahib al Jawahir alifanya uhakiki mkubwa wa masuala ya fiqhi na kusajili fi

SASA NI ROBO FAINALI

Image
Wachezaji, maafisa na mashabiki wamepata mapumziko mafupi katika fainali za ubingwa wa Ulaya,Jumatano ,(20.06.2012), lakini manung'uniko ya Ukraine ambayo ni mwenyeji mwenza wa mashindano haya yanaendelea. Ukraine wamejiunga  na  wenyeji  wenza  Poland  kuwa  ni  pumba   katika mashindano  haya   baada  ya  kushindwa  kwa  bao  1-0  dhidi  ya Uingereza  na  gumzo  lilituwama  katika  goli  ambalo  halikuwa, ambalo  refa  aliamua  kuwa  halikuvuka  mstari  lililofungwa  na wenyeji  hao  dhidi  ya  Uingereza. Haki haikutendeka Hisia  za  kutotendewa  haki  nchini  Ukraine  hazikuweza  kupozwa na  Pierluigi Collina, mkuu  wa  waamuzi  katika  shirikisho  la kandanda  barani  Ulaya  Uefa, kwa  kukiri  kuwa  goli  lile  lilipaswa kukubaliwa. Mkuu wa marefa wa Uefa Pierluigi Collina Ukraine  pia  bado  inaendelea  kupambana  na  maandamano kuhusiana  na  kufungwa  kwa  waziri  mkuu  wa  zamani  Yulia Tymoshenko , wakati  serikali

MIZENGWE YAENDELEA MISRI

Image
Tume ya uchaguzi nchini Misri imeahirisha kutangaza matokeo ya uchaguzi wa rais nchini humo yaliyotarajiwa Alhamis (21.06.2012), ili kushughulikia malalamiko yaliyotolewa na wagombea wa kiti hicho. Tume hiyo ilitangaza Jumatano jioni kupitia televisheni ya taifa kuwa inangalia malalamiko karibu mia nne yaliyotolewa na Muhammed Mursi na Ahmed Shafique, lakini haikusema ni lini itatangaza mshindi. Mursi na Shafique wote walijitangazia ushindi. Tangazo hilo limeongeza hali ya wasiwasi nchini Misri wakati ambapo Mohammed Mursi anadai kuna njama zilizoandaliwa dhidi ya chama chake cha udugu wa Kiislam ili kuvuruga uchaguzi na kumtupa nje ya kinyanganyiro hicho. Wandamanaji wakiwa katika uwanja wa Tahrir mjini Kairo siku ya Jumatano. Shutuma hizo zinazidisha munkari na uwezekano wa kutokea sintofahamu kwa upande wa chama hicho endapo mpinzani wa Mursi, Waziri Mkuu wa mwisho wa Hosni Mubarak atatangazwa kuwa mshindi wa kiti cha urais. Tangazo

SAMARAS NDIYE WAZIRI MKUU MPYA WA UGIRIKI

Image

Maharamia wateka meli ya Italia

Image
Jeshi la wanamaji la Italia limesema maharamia wamekwea na kuchukua udhibiti wa meli ya mafuta ya Italia katika bahari ya Hindi. Meli ya Ujerumani ambayo pia imetekwa Maharamia hao walifyatua risasi katika chombo kiitwacho Savina Caylyn, takriban kilomita 800 kutoka pwani ya Somalia. Msemaji wa jeshi la wananamaji amesema hakuna aliyejeruhiwa miongoni mwa mabaharia 17 kutoka India na wataliano watano. Maharama wamejipatia mamilioni ya dola Msemaji wa jeshi la wanamaji la Umoja wa Ulaya amesema shambulio la chombo hicho limefanyika katika eneo la mashariki mwa kisiwa cha Yemen cha Socotra. Meli hiyo imebeba shehena ya mafuta yaliyokuwa yakipelekwa katika bandari ya Pasir Gudang nchini Malaysia, limeripoti shirika la habari la Reuters. Wanajesh

WAWILI WAACHILIWA SOMALIA

Image
Raia wawili wa Afrika Kusini ambao wamekuwa wakishikiliwa mateka na Maharamia wa Kisomali wameachiliwa huru. Wawili hao, Bi Calitz na Bwana Pelizzari, ambao ni mtu na mkewe wamekuwa wakizuiliwa nchini Somalia kwa miezi 20 Waziri wa ulinzi wa Somalia amesema jeshi na walinda usalama walikuwa wameanza harakati za kuwaokoa watu hao siku ya Jumatano usiku. Bi Calitz na Bwana Pelizzari walitekwa nyara mwezi Oktoba mwaka 2010 walipokuwa ndani ya chombo chao katika bahari hindi. Hata hivyo Waziri wa ulinzi wa Somalia Hussein Arab Isse hakufichua kama kikombozi chochote kililipwa kabla ya wawili hao kuachiliwa. Awali maharamia hao walikuwa wametaka kulipwa dola milioni 10 kabla ya kuwaachilia raia hao wawili wa Afrika Kusini. Mtu huyo na mkewe walijitokeza wakiwa na waziri huyo katika mkutano wa waandishi habari. Walisema walikuwa na furaha na waliku

WASHINDI WENGINE WANNE WASHINDA ZAWADI ZA SBL

Image
Kampuni ya bia ya Serengeti imekuwa ikizunguka katika mikoa mbalimbali hapa nchini kukabidhi zawadi kwa washindi wa zawadi hizo katika promosheni inyoendelea’VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO NA SBL, inayoendeshwa na kampuni hiyo kwa kipindi cha wiki 7 sasa na kubakisha takribani wiki 9 ili kuisha kwa promosheni hiyo ya kipekee kabisa kutokea hapa nchini Tanzania   hakika watanzania wengi wananufaika na kupiga hatua mbele kimaisha.A Asubuhi ya leo droo ya nne katika promosheni hiyo ‘VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO’ imechezeshwa katika ofisi za kampuni ya bia ya Serengeti SBL zilizopo maeneo ya Oysterbay jijini na kuhudhuriwa na waandishi wa habari, wasimamizi kutoka Bodi ya Bahati Nasibu Tanzania, wadau kutoka ndani na nje ya kampuni hiyo, wakiwemo kampuni ya kuendesha Bahati Nasibu ya PUSH MOBILE, wahakiki na wakaguzi kutoka PWC-Price Water House Coopers. Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia vinywaji vyake aina ya Serengeti premium Lager, Tusker Lager na Pilsne

WENGI WAMUAGA WILLY EDWARD OGUNDE

Image
 Prof. Ibrahim  Lipumba kushoto Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF, Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, na Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP Bw. Reginald Mengi wakijumuika pamoja na viongozi wengeni, ndugu jamaa na marafiki pamoja na waombolezaqji wengine walioudhuria katika ibada ya  kuaga mwili wa marehemu Willy Edward Ogunde aliyekuwa mhariri mkuu wa Gazeti la  Jambo leo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam jana. Mwili wa marehemu Willy Edward Ogunde aliyekuwa mhariri mkuu wa Gazeti la  Jambo leo ukiwasili  katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam jana. Mjane wa Marehemu Willy Edward Bi Rehema akifarijiwa na ndugu huku akilia kwa uchungu kwa kumpoteza mume wake mpendwa marehemu Willy Edward. Mwenyekiti wa IPP Reginald Abraham Mengi , Akimfariji Athumani Hamisi katika msiba huo Mwenyekiti wa makampuni ya  IPP Reginald Abraham  Mengi , Akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Willy Edward wan

KONGAMANO LA MICHEZO KUANZA KESHO

Image
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Leonard Thadeo akiongea na waandishi wa habari (hawapo Pichani) juu ya Kongamano la Michezo kwa maendeleo na amani litakalofanyika jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Blue Pearl,Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Right to play Josephine Mukakalasi na kulia ni Meneja mradi Bw. George Agango kutoka British Council.Kongamano hilo limeandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Habari na Taasisi hizo.Picha na (Benjamin Sawe wa WHVUM)   Na Concilia Niyibitanga- WHVUM   Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kushirikiana na taasisi za Right To Play na British Council zimeandaa Kongamano la Michezo kwa Maendeleo na Amani linalotarajia kuanza kesho  katika Hoteli ya Blue Pearl kuanzia 3: 00 asubuhi.   Akiongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Bw. Leonard Thadeo amesema lengo kubwa la Kongamano hilo ni kutoa fursa kwa wadau mbalimbali kubadilishana mawazo,

TANGAZO KWA WANAFUNZI WALIOHITIMU KWENYE VYUO VYA AFYA MACHI,2012

Image
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kuwajulisha  wanafunzi wote waliohitimu  vyuo vya afya nchini mwezi Machi 2012, kufika Wizarani ili waweze kuchukua barua za kupangiwa vituo vya kazi kabla ya tarehe 30 June,2012. Pia waombaji wengine waangalie majina yao kwenye website ya Wizara www.moh.go.tz Imetolewa na: Regina L. Kikuli Kaimu Katibu Mkuu 21/06/2012

WAREMBO MISS DAR INTERCOLLEGE WAFUNDWA

Image
KAMATI ya Miss TAnzania jana imetembelea kambi ya Miss Dar Intercollege iliyopo kwenye hoteli ya The Grand Villa, Kijitonyama jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwafunda. Shindano hilo linatarajiwa kufanyika ijumaa ya kesho katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa uliopo mkabala na chuo cha Usmiamizi wa Fedha (IFM). Akizungumza na warembo hao, mkuu wa Itifaki wa Kamati ya Miss Tanzania Albert Makoye aliwataka warembo hao kufuata miongozi na kanuni za shindano hilo ikiwemo kuwa na nidhamu. Alisema urembo si sura na umbo zuri bali unahusisha pia nidhamu katika jamii hivyo amewataka warembo hao kuzingatia hayo. "Nafahamu ninyi ni wasomi wazuri hivyo mmeyapokea vema mafunzo tuliyowapa...hatutarajii kusikia mmoja wenu anachafua hali ya hewa katika siku za usoni na mambo ya skendo skendo,"Alisema Makoye. Dina alisema shindano hilo litapambwa na msanii wa uziki wa kizazi kipya nchini Nasib Addul ‘Diamond’ sambamba na  bendi ya Skylight iliyopo

MKUU WA WILAYA YA MERU ATOA WITO WA KUANZISHA KITUO CHA TELEVISHENI

Image
MKUU wa wilaya ya Arumeru Bw Nyerembe Munasa ametoa changamoto kwa halimashauri ya Meru na  manispaa  ya Arusha kuanzisha television za halimashauri ambazo zitawawezesha kuandaa program ambazo zitawaelekeza wananchi wao kutambua mambo muhimu yanayoendela katika halimashauri zao pindi wawapo kwenye vikao Bw. Nyerembe aliyasema hayo alipokuwa akiongea katika semina ya wadau wa hlimashuri hizo ya  kuelimisha umma kuhusiana na mabadiliko ya mfumo wa utangazaji kutoka analojia kwenda digital iliyofanyika mjini hapa. Bw. Nyerembe amesema kuwa  kutokana mabadiliko ya mafumo wa utangazaji halimashauri zinapaswa kuhakikisha kuwa zinaanzisha television ambapo kupitia mfumo huo zitawawezesha wananchi kuelewa mambo yanayoendelea katika halimashauri zao pindi wawapo kwenye shughuli zao. Aidha amewataka madiwani  wa halmashauri hizo kuhakkisha kuwa wanasimamia kikamilifu miradi ya wananchi hao na kuhakikisha kuwa wanawapa taarifa sahihi za mabadiliko ya mfumo wa utangazaji . Mba

MPANGO WA NMB FINANCIAL FITNESS WAENDELEA

Image
 Dotto Mbwana, mfanyakazi wa NMB Muhimbili akigawa vijarida vya NMB Financial Fitness kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Muhimbili mpango huo ni kwa ajili ya kuwaandaa wanafuzi kupata uelewa wa masuala ya kibenki mashuleni Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mtibwa wakijisomea kijarida cha NMB Financial Fitness wakati wafanyakazi wa NMB Turiani walipotembelea shule yao  Wanafunzi wa Shule ya Msingi Muhimbili wakisoma kijarida cha NMB Financial Fitness  Wanafunzi wa Shule ya Msingi Muhimbili wakisoma kijarida cha NMB Financial Fitness Meneja wa NMB Muhimbili Janeth Shango akiwasisitizia wanafunzi juu wa kuweka fedha wakiwa na umri mdogo

IRINGA ASUBUHI YA LEO

Image