Posts

Showing posts from June 9, 2012

TSN HAIJAMTELEKEZA ATHUMANI HAMISI

Image
Tarehe 5 Juni,2012, mfanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), ambaye amelemaa baada ya kupata ajali ya gari, Bwana Athumani Hamisi, aliitisha mkutano wa waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Maelezo, Dar es Salaam, na kutoa taarifa iliyojenga taswira kuwa ametelekezwa na TSN pamoja na Serikali. TSN inapenda kufafanua kuwa Serikali na kampuni hii, ambayo ilimwajiri Athumani tarehe 1/09/2006 kama Mpiga picha Mwandamizi, wamemhudumia mfanyakazi huyo kikamilifu tangu alipopata ajali tarehe 12 Septemba, 2008 hadi sasa, na huduma hiyo inaendelea. Baada ya kutokea ajali hiyo, TSN kama mwajiri ilisimamia matibabu yake ya awali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Kitengo cha Mifupa (MOI) mpaka Serikali, kwa kupitia Wizara ya Afya ilipomhamishia Netcare Rehabilitation Hospital nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi. Serikali ililipia gharama za matibabu yake yote akiwa Afrika Kusini kwa kipindi cha mwaka mmoja na miezi saba, ambayo yanazidi shilingi milio
Image
MAMLAKA ya maji safi na maji taka Jijini Arusha(AUWSA ),imebaini kuhujumiwa wa watu mbalimbali wakishirikiana na wafanyakazi wake, wasio waaminifu kwa kuunganisha maji kinyume cha utaratibu na kusababisha upotevu mkubwa wa mapato. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa AUWSA, Eng.Ruth Koya alisema kuwa, tayari wamefanikiwa kuwanasa wezi wa maji zaidi ya 100 waliojiunganishia kinyume na utaratibu, wakiwemo vigogo wa halimashauri ya Arusha,ambao wamekuwa wakitumia huduma hiyo kwa kipindi kirefu,bila kulipa chochote na kuisababishia hasara kubwa mamlaka hiyo. Vigogo wa halmashauri waliokamatwa ni pamoja na Afisa mali asili, mazingira na ardhi, Maico Myairwa ambaye yeye aling’oa kabisa mita ya idara ya maji, ambayo imekutwa chumbani mwake, ameificha huku akijua ni kosa kisheria. Mwingine ni fundi mkuu wa maji wa halmashauri ya Arusha,Loishono Mollel ambaye amejiunganishia maji baada ya kutoboa bomba kubwa la idara ya maji na kupitisha mpira mrefu kwa chini, hadi nyumbani kwake a

MKUU WA MKOA WA ARUSHA

Image
Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa mulongo Na Ashura Mohamed,Arusha VIONGOZI wa serikali pamoja na wa madhehebu ya dini wametakiwa kutambua kuwa wana wajibu mkubwa wa kubadili mitazamo na imani kwa wananchi wao wanaowaongoza ikiwa ni pamoja na kuwa wawazi na wawajibikaji ili pawe na utawala bora katika jamii. Hayo yalisemwa na mkuu wa wilaya ya mbeya Dk Norman Sigala wakati alipokuwa akiongea katika mdahalo wa umma unahousu uwazi na uwajibikaji wa viongozi na watendaji wa serikali katika kusimamamia rasilimali za umma uliandaliwa na muungano wa asasi za kiraia( Angonet) na kufanyika mjini hapa. Alieleza kuwa ni vema viongozi wakawa na maadili na wakahakikisha kuwa wanatenda haki kwa wananchi wao kwa kuwa wawazi kwa mambo mbali mbali wanayoyafanya ili kuwaepusha na migogoro mbali mbali inayotokea baina yao na wananchi. “Endapo viongozi watakuwa wawazi kuwaeleza wananchi wao mambo yanayoendelea katika halmashauri zao itasaidia kuelewa matatizo na mafanik

NGOWI KUONGOZA KAMATI YA KUONGOZA YA KUANDAA MKUTANO 30 WA SHIRIKISHO MWAKANI

Image
Kushoto ni Rais wa IBF/USBA katika bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi Onesmo Ngowi akimkabidhi cheti cha kutukuka Rais wa Shirikisho hilo duniani Daryl Peoples wa Marekani katika sherehe iliyofanyika kwenye Hotel ya Hawaiian Hilton Village Resort, jijini Hawaii, nchini Marekani. Habari na picha zi metumwa toka katika jiji la Honolulu, Hawaii, Marekani Shirikisho la Ngumi la Kimataifa na Chama cha Ngumi cha Marekani (IBF/USBA) limeteua Rais wa Shirikisho hilo katika bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi,   Mtanzania Onesmo Ngowi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kuandaa mkutano wa 30 wa Shirikisho hilo mwakani. Mkutano wa 30 wa IBF/USBA unatarajia kufanyika katika jiji la Berlin nchini Ujerumani kuanzia tarehe 24 hadi 30 Juni mwaka 2013. Ngowi alichaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa shirikisho la IBF/USBA uliomalizika Hilton Hawaiian Village Resort, jinini Honolulu, Hawaii, Marekani tarehe 2 Juni. Uteuzi wa Ngowi unafuatia juhu

MAXIMO KUJA JANGWANI?

Aliyewahi kuwa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Marcio Maximo, anatarajia kutua nchini wiki ijayo kwa ajili ya kutua Klabu ya Yanga na kuchukua mikoba ya Kocha anayemaliza muda wake katika Klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam imeelezwa. Kocha huyo anatarajia kuwasili nchini akiwa na Kocha msaidizi wa Viungo, huku akiwa ameongozana na mkewe kutokana na kuwa nashughuli pevu ya kukiandaa kikosi hicho cha Yanga kinachotarajia kushiriki michuano ya Kombe la Kagame. Aidha imeelezwa kuwa mara tu baada ya kupokea maombi ya kukinoa kikosi hicho Maximo hakuwa na pingamizi lolote bali alikubaliana na maombi hayo moja kwa moja huku akitoa mapendekezo ya kuwasajili wachezaji awatakao kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Katika mapendekezo hayo ya wachezaji aliowahitaji Maximo ni pamoja na Beki wa Simba, ambaye hadi sasa bado anazua gumzo na mtafaruku mkubwa baina ya Klabu hizo mbili za watani wa jadi Simba na Yanga, Kelvin Yondan, pamoja

MKAZI WA MBEYA KAMA ALIVYOKUTWA JANA

Image
 Muuza Miwa maarufu akiwa anakatiza West Street jijini Mbeya  mapema leo   Muuza Miwa maarufu akiwa anapanga miwa yake leo   Miwa ikiwa tayali kwa ajili ya kufanyiwa mauzo leo   Mwandishi Mkuu wa Mbeya yetu Blog  Joseph mwaisango aliye vaa shati Jeupe akifanya mahojiano na Muuza miwa huyo   Muda mchache baada ya kufanya mazungumzo Wadau walianza nunua Miwa eneo hilo   Mwandishi wa Mbeya yetu Joseph Mwaisango Kulia akiwa na muuza miwa Pamoja na mdau mwengine wakipata miwa kutoka kwa mdau Baada ya Mazungumzo na Mbeya yetu mdau aliondoka zake *********************** Mbeya yetu leo katika Kodoa kodoa na Kamera yetu ilipaya bahati kuonana Live na Bwana Mecky ambaye ni muuza Miwa maarufu jijini Mbeya. Ambapo alipo hojiwa alisema "Kwa kweli miwa hii naifuata kule Usangu ambapo nanunulia kwa bei ya kule kule, Lakini miwa hii pia huwa naisambaza hapa jijini pamoja na vitongoji vyake". Aliongeza na kusema kuwa "Watu wengi wanaidharau sana  bia

AJARI

Image
 Gari la Fusso lililo sababisha Ajali hiyo   Namba za gari la Fusso  Toyota Rav 4 ikiwa imebamizwa vibaya na Fusso hilo   Gari la Rav 4 lilivyo haribika kwa nyuma  Namba za Gari la Rav 4  Fusso kwa nyuma   Fusso kwa Mbele  *********************************** Ajali Mbaya imetokea usiku huu iiyo husisha Gari la Fusso namba T 596 BUB pamoja na Rav 4 namba  T 675 ATK, Maeneo ya CCM Mkoani Mbeya.  Shahidi aliye kuwepo eneo la tukio amedai  ya kuwa Dereva wa Gari la mizigo Fusso alikuwa mwendo kasi sana, na huku akijaribu kuyapita magari mengine matano ambayo yalikuwa mbele yake. Wakati huo anaendelea kuyapita magari hayo tayali dereva wa Rav 4 alikuwa amesha washa taa kuonesha kuwa anaelekea kulia na ndipo Dereva wa fusso akaligonga Gari la Rav 4 ambalo baada ya hapo liliseleleka kwa umbali wa Takribani mita 300 kutoka usawa wa sehemu ambapo liligongewa.  Hata hivyo dereva wa Fusso aliyesababisha Ajali hiyo amekimbia eneo hilo. Hakuna aliye um