Posts

Showing posts from June 28, 2012

Wahamiaji 42 wafa kwenye lori Tanzania

Image
Tanzania Wahamiaji haramu arobaini na wawili wamepatikana wakiwa wamekufa ndani ya lori walimokuwa wakisafiria katika mkoa wa Dodoma, nchini Tanzania. Naibu waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania, Pereira Silima, amesema kuwa watu hao waliokuwa wamesongamana ndani ya lori waliaga dunia kutokana ukosefu wa hewa safi. ''Taarifa tuliyopata ni kwamba kulikuwa na wasafiri waliokuwa wakisafirishwa kwenye lori, ambalo lilikuwa kama kontena na halikuwa na hewa ya kutosha''.Bwana Silima ameambia BBC. wahamiaji walikuwa wanatoka Ethiopia Amesema wahamiaji hao haramu kutoka Ethiopia walikuwa wakijaribu kuingia Malawi. Kulingana na bwana Silima wahamiaji hao walianza kufariki dunia wakiwa safarini. Jihudi za wahamiaji hao kumjulisha dereva kuhusiana na hali yao hazikufanikiwa, na hivyo kusababisha maafa ya watu arobaini na moja ndani ya lori hilo. Kulingana na naibu waziri huyo wa mambo ya ndani tukio hilo lilifanyika Jumatatu usiku. Na ba

Ufadhili wa silaha waleta vita S Sudan

Image
Wanajeshi wa Sudan Kusini Silaha kutoka China, Ukraine na Sudan zinachangia machafuko Sudan Kusini. Hii ni kwa mujibu wa Shirika la Kutetea Haki za Binadamu, Amnesty International. Ripoti ya shirika hilo imesema raia wameendelea kuawa na kujeruhiwa kiholela kwenye makabiliano kati ya kundi moja la waasi na jeshi la Sudan Kusini. Amnesty International inasema silaha kutoka Sudan, mabomu ya kutegwa arthini kutoka China na Vifaru vilivyoagizwa Ukraini zimeendelea kutumiwa nchini humo. Hakuna upande ambao umejibu madai ya ripoti hii.   Vifaru vya Jeshi la Sudan Kusini vilitolewa kwa lililokua kundi la SPLA kati ya mwaka 2007 na 2009 kutoka Ukraine na kupitishiwa Kenya.Shirika hilo linaendelea kusema ,kampuni za Ujerumani na Uingereza ndizo zilihusika na usafirishwaji wa silaha hizo. Kutolewa kwa silaha hizo kulifanyika licha ya kuwepo mkataba wa amani wa mwaka 2005 pamoja na marufuku ya silaha iliyowekewa Sudan nzima.Ripoti ya Amnesty International imen

CHAMELEONE KUTUA BONGO

Image
Msanii wa Uganda, Jose Chameleone (pichani juu) leo amekamilisha taratibu zote za kusaini mkataba wa kufanya shoo kali Uwanja wa Taifa mpya, jijini Dar es salaam, siku ya sabasaba baada ya Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho, kutia timu Entebe mapema leo. Pichani chini ni Chameleone akijigamba kufanya shoo na akisaini mkataba wa mwisho huku akishuhudiwa na meneja wake. Chameleone ametoa onyo kwa Diamond kuwa atamchakaza na Valuvalu!

FFU KUVAANA NA WASHABIKI

Image
Mjini Dortmund, Ujerumani jumamosi 30 Juni 2012 Kikosi kazi cha Ngoma Africa Band aka FFU bendi yenye makao yake kule Ujerumani,wanategemewa kukwea jukwaa la Afro-Ruhr Festival, siku ya jumamosi 30 Juni 2012 mjini Dortmund,Ujerumani. Bendi hiyo maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya inayoongozwa na mwanamuziki Ebrahim Makunja aka kamanda Ras Makunja wa FFU,itapeleka mzimu wake wote wa dansi katika onyesho hilo kubwa la aina yake,washabiki wa muziki katika onyesho hilo wanakumbana "Jino kwa Jino" na makombora ya muziki wa Ngoma Africa band aka FFU, bendi hiyo kwa sasa inatamba nyimbo zake za "Supu ya Mawe" ,"Uhuru wa Habari" na "Bongo Tambarare" ambazo ipo katika CD ya "BONGO TAMBARARE" pia zinasikika katika kambi yao FFU