Posts

Showing posts from June 13, 2012

BIA RUHUSA KOMBE LA DUNIA BRAZILI

Image
Rais wa Brazil Dilma Rousseff amesaini kuwa sheria muswada utakaoruhusu uuzwaji wa bia wakati wa mechi za Kombe la Dunia mwaka 2014. Rais wa Brazil akiwa na viongozi wa Fifa pamoja na Pele Shirikisho la Kandanda Duniani, Fifa, lilikuwa linataka mabadiliko katika sheria ya Brazil inayopiga marufuku pombe kuuzwa kwenye mechi za mpira wa miguu. Muswada huo mpya, umeweka sheria kadha kwa ajili ya Kombe la Dunia, haujaelezea kuweka pingamizi lolote la kuuzwa pombe. Waandishi wa habari wanasema magavana wa majimbo bado wanaweza kupiga marufuku uuzwaji wa bia wakati wa mashindano hayo. Uuzaji bia umekuwa mwiko katika mechi za kandanda nchini Brazil tangu mwaka 2003. Upigwaji huo marufuku uliwekwa ikiwa ni sehemu ya hatua ya kupambana na vurugu miongoni mwa mashabiki wa timu zenye uhasama pamoja na kukabiliana na wahuni
Image
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amemfuta kazi mkuu wa polisi Generali Bheki Cele, aliyekuwa ametuhumiwa kwa makosa ya rushwa. Bwana Zuma aliambia waandishi wa habari kuhusu uamuzi wake na pia kuhusu atakayechukua nafasi yake akiwa ni bwana Mangwashi Phiyega. Hatua hii inamfanya bi Mangwashi kuwa mkuu wa kwanza wa polisi mwanamke. Generali Cele, ambaye mtangulizi wake alifungwa jela kwa tuhuma za ufisadi, alihukumiwa mwezi Oktoba baada ya taarifa kuhusu kuhusika kwake katika kashfa uuzaji haramu wa nyumba za polisi ingawa alikanusha madai hayo. Inaaminika alihusika na kampeini ya rais Zuma wakati wa kampeini za uchaguzi wa rais mwaka 2009. Mwaka jana afisa anayechunguza kesi za ufisadi ,Thuli Mandonsela, alisema kuwa nyumba za polisi zilikodiwa kutoka kwa kampuni moja ambayo ilipandisha bei ya kukodi na kwamba Cele ndiye alihusika na kashfa ya

KESI YA LULU YASOGEZWA HADI JUNI 25

Image
WAKILI mmoja wapo anayemtetea  Elizabeth Michael  Fulgence Massawe akimsalimia ''maarufu kama  Lulu'' kabla Jaji Dk. Fauz Twaibu hajaingia Mahakamani juzi asubuhi katika Mahakama Kuu ambako kesi hiyo ilipigwa tena kalenda hadi Juni 25 mwaka huu. Pia Jaji Fauz amezitaka pande zote mbili yaani Wakili wa Serikali pamoja na Jopo la Mawakili wanaomtetea  kupeleka vuthibitisho kuhusiana na umri wa Lulu Mahakamani hapo. MAHAKAMA Kuu kanda ya Dar es Salaam imewataka mawakili wa utetezi na jamhuri kuwasilisha uthibitisho kuhusu umri wa msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ kabla ya kutoa uamuzi wake Juni 25, 2012. Agizo la Mahakama hiyo lilitolewa juzi na Jaji Dk. Fauz Twaib anayesikiliza madai ya utata wa umri wa msanii huyo nyota wa maigizo nchini. Kabla ya kuahirisha kesi hiyo Jaji Dk. Twaib alizitaka pande mbili zinazobishana kupeleka vithibitisho vya hati ya kiapo cha cheti cha kuzaliwa ili kujiridhisha umri sahihi wa Lulu.

MATUKIO MBALI MBALI YA BUNGENI JANA

Image
Waziri Mkuu, Mizengo pinda  akizungumza na  Mbunge wa Viti Maalum  Pauline Gekul na watoto wake Irene (kushoto)  na Inocentia kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 12,2012. Spika wa Bunge Anne Makinda akimkabidhi kanuni za Bunge Mbunge wa Kuteluliwa James Mbatia baada ya kumwapisha, Bungeni Mjini Dodoma, Juni 12,2012. Mbunge wa Kuteuliwa Janet Zebedayo Mbene akiapa, Bungeni Mjini Dodoma  Juni 12, 2012. Mbunge waKuteuliwa Saada  Mkuya  Salum akiapa Bungeni Mjini Dodoma Juni 12, 2012. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza na Mbunge wa Namtumbo Vita Kawawa (kushoto) na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu  Nchemba kwenye viwanja vya Bunge Mjini  Dodoma  Juni 12, 2012. Mbunge wa Kuteuliwa, Sospeter  Mwijarubi Muhongo akiapa, Bungeni Mjini Dodoma, Juni 12, 2012.

MAJUMBA SITA WAFUNGA BAARABARA

Image
 Wakazi wa Eneo la Ukonga Majumba Sita Wilaya ya Ilala jijini Dar es sal;aam leo walifunga barabnara kuu ya Nyerere katika eneo hilo la majumba sita kushinikiza kuwekwa kwa matuta katika eneo hilo kufuatia kukuthiri kwa ajali za wakazi wa eneo hilo kugongwa wavukapo barabara hiyo. Tukio hilo lilitokea leo majira ya saa za asubuhi na kudumu hadi saa nane mchana baada ya kijana mmoja kungongwa katika eneo hilo akijaribu kuvuka barabara hiyo na kufa papo hapo. Wakiwa na mabango, mawe na matofali wakazi hao waname, wanawake, wazee kwa watoto walifurika katika barabara hiyo na kushinikiza kuja kwa mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuwekwa kwa matuta.  Wananchi wakiwa wamefurika kwa wingi barabarani na hata Jeshi la polisi lililopfika na kuwasihi waruhusu magari kupita waligoma na huko mitaani pia walizuia boda boda (pikipiki) kupita hadi matuta yawekwe.  Magari yakiwa yamezuiwa eneo hilo karibu na Kambi ya Jeshi Kikosi cha Anga.  Wananchi wakiwa upande

EXIM BANK AT REAL ESTATE TANZANIA HOME EXPO EXHIBITION

Image
The Exim Bank’s M anaging Director, Anthony Grant (L) greets the Vice President of the United Republic of Tanzania, Dr Mohammed Gharib Bilal when he visited the Exim Bank tent during the official launch of the real estate exhibition dubbed Tanzania Homes Expo Exhibition held at Mlimani City in Dar es Salaam over the weekend. Centre is the bank’s Head of Retail Banking Depa rtment, Ramakrishna Rao. (Photo by Our Correspondent). The Exim Bank’s Managing Di rector, Anthony Grant stressing a point to Vice President of the United Republic of Tanzania, Dr Mohammed Gharib Bilal when he visited the Exim Bank tent during the official launch of the real estate exhibition dubbed Tanzania Homes Expo Exhibition held at Mlimani City in Dar es Salaam over the weekend. Centre is the bank’s Head of Retail Banking Department, Ramakrishna Rao. (Photo by Our Correspondent).

SCF YAZINDUA MFUMO WA UTOAJI HABARI ZA MASOKO

Image
Mkurugenzi wa Mradi Mfuko wa Kukuza Ushindani kwa Wazalishaji wa Kati na Wadogo (SCF), Casmir Makoye akitoa maelezo kuhusu matumizi ya mfumo utaoonyesha habari muhimu kuhusu masoko (Point of Sale (POS) datacbase) ambao utaangaza masoko ya Dar es Salaam na Zanzibar uliyozinduliwa jana Jijini Dar es Salaam. Waliokaa ni wawakilishi wa makampuni madogo na ya kati yanayosindika na kuuza vyakula. Picha na mwandishi wetu. Na Mwandishi Wetu MFUKO wa Kukuza Ushindani kwa Wazalishaji wa Kati na Wadogo (SCF) umezindua mfumo utaoonyesha habari muhimu kuhusu masoko ambao utaangazia masoko ya Dar es Salaam na Zanzibar. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, mjini Dar es Salaam, jana, Mkurugenzi wa Mradi huo, Casmir Makoye, alisema huduma hiyo inawalenga wajasiriamali wadogo na wa kati ambao husindika na kuuza vyakula. Makoye alisema uzinduzi huo unatokana na maombi ya wajasiriamali wengi kutaka kufanya utafiti wa masoko ambao umekuwa na gharama kubwa. Awali, k

DIWANI WA KATA YA KIGAMBONI KUWA MGENI RASMI MISS KIGAMBONI CITY

Image
DIWANI wa Kata ya Kigamboni kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dotto Msawa, atakuwa mgeni rasmi katika shindano la urembo la kitongoji cha Kigamboni mwaka huu ' Redd's Miss Kigamboni 2012' ambalo litafanyika kesho Ijumaa kwenye ukumbi wa Navy Beach jijini Dar es Salaam. Akizungumza jana jijini, Mratibu wa shindano hilo, kutoka kampuni ya K&L Media Solutions, Somoe Ng'itu, alisema jana kuwa maandalizi ya zoezi hilo yamekamilika na wanamshukuru diwani huyo pamoja na diwani wa Vijibweni (CCM), Suleiman Mathew, kusaidia maandalizi ya shindano hilo. Alisema kuwa warembo 12 kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini wanatarajia kuchuana kuwania taji hilo na anaamini kwamba kitongoji hicho kimepania kurudisha taji la Miss Tanzania kwenye Kanda ya Temeke. Aliongeza kuwa ili kuboresha shindano hilo bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia maarufu Wazee wa Ngwasuma na msanii na mchekeshaji mahiri hapa nchini, Mpoki watatumbuiza kwenye kinyang'anyiro hicho. Aliwaomba

H.BABA APAGAWISHA TAMASHA LA TIGO WILAYANI BABATI

Image
Msanii wa muziki wa kizazi kipya H,Baba akifanya mambo yake wakwati alipotoa burudani kwenye promosheni ya tamasha la Tigo ilofanyika katika viwanja vya wilayani Babati ambapo  wateja wa Tigo walijipatia zawadi mbalimbali zikiwemo simu, Tishirt na kofia. Ziara hiyo ya Tigo itanayoendelea  kufanyika katika mikoani mbalimbali. Baadhi ya watu kutoka seemu mbalimbali  wilayani Babati wakifuatilia kwa umakini burudani iliyokuwa ikitolewa msanii wa mziki H Baba.

WANAWAKE KIJIJI CHA IFIGO MBEYA WADAI MAJI

Image
WANAWAKE wa kijiji cha Ifiga kata ya Ijombe wilaya ya Mbeya mkoani Mbeya wamedai kuwa tatizo la maji katika kijiji hicho limeendelea kuwa sugu na kupelekea kutumia maji ya kisima ambayo si safi na salama na kujikuta wakiendelea kukumbwa na tatizo la ugonjwa wa kichocho . Wakizungumza na timu ya wanahabari wanaharakati wa mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) waliotembelea kijijini hapo leo wanawake hao walisema kuwa kijiji hicho kutokana na ukosefu wa huduma hiyo ya maji wamekuwa wakilazimika kuchota maji katika kisima kimoja kilichoppo kijijini hapo ambacho maji yake si lazima kwa afya za binadamu. Alisema Sophia John kuwa kisima hicho kimekuwa kikitumia na wakazi zaidi ya 2000 wa kijiji hicho na kuwa pamoja na kuwa maji hayo si salama baadhi ya watu hasa watoto wamekuwa wakiyanywa pasipo kuchemcha hali inayochangia kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa wa kichocho katika kijiji hicho. John alisem

MABALOZI WAPYA WALAKIWA

Image
Kutoka kulia ni balozi Dora Msechu,balozi Irene Kasyanju,balozi Bertha Somi, na balozi Naim Azizi.