Posts

Showing posts from June 6, 2012

HARAMBEE

Image
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa  na  Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi (kushoto)  na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa baada ya kuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia Taasisi ya Mkapa HIV/AIDS foundation na kusaidia  kukusanya shilingi bilioni 3.2 nauvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita (PICHA NA IKULU) Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Bw. Deo Mwanyika, Makamu wa Rais wa Kampuni ya Barrick Tanzania baada ya kuibuka mchangiaji mkubwa kwa kutoa dola za Kimarekani laki 5 kwa ajili ya kuchangia taasisi ya Mkapa Hiv/Aids Foundation Jumanne Juni 5, 2012 usiku katika hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam. Kushoto ni Rais Mstaafu  wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa aliyeandaa hafla hiyo iliyoweza kukusanya shilingi bilioni 3.2 na kuvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita  Rais Jakaya Kikwet

SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA ANNA MAKINDA AKIAGANA NA BALOZI WA MSUMBIJI ANAYEMALIZA MDA WAKE

Image
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimsikiliza kwa makini Balozi wa Msumbiji hapa Nchini Mhe. Amour Zacarias Kupela, wakati alipofika Ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake nchini.

JK AKUTANA NA VIONGOZI WA KAMPUNI YA YARA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na viongozi wa kampuni ya kilimo ya YARA  ya nchini Norway inayoshughulika na uzalishaji wa mbolea wakati walipomtembelea ikulu jijini Dar es Salaam leo.Kampuni hiyo ina andaa mipango ya kuzalisha mbolea nchini. (PICHA NA IKULU) Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kampuni ya Kilimo ya YARA ya nchini Norway wakati alipomtembelea ikulu jijini Dar es Salaam leo

INTERVIEW WITH COMEDIAN EVANS BUKUKU

Image
Just a couple of years ago, stand-up comedy were not very popular in Tanzania. In fact, it was almost non-existing. If it was, then it was done in very informal settings such as in the streets or local bars and not so much in prearranged settings whereby the audiences are well seated and eagerly waiting to be entertained and laugh to the point of shedding those tears of a good laugh. I am talking about the laugh that makes your entire body vibrate like a Samsung’s hand held gadget! However, the above scenario of lack of organized stand-ups is changing or has changed. Thanks to one man who, according to his own words, he is almost on a “crusade” to change how and where we can go and have a good laugh. His name is Evans Bukuku. He is now, by far, the new face or our own definition of Stand-Up comedy in Tanzania. He is best known for his once a month(every last Tuesday of the Month) smart and hilarious stand-up comedy routines  that features him making funny

VIONGOZI WA BENDI ZA DANSI WAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI

Image
Kiongozi wa Bendi ya Muziki wa dansi ya Extra Bongo, Ally Choki (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu mkutano utakao husisha bendi mbalimbali na wadau wa muziki huo wenye lengo la kuinua wanamuziki chipukizi kupitia vyombo vya habari na masuala mengine. Kushoto ni mmoja wa kiongozi wa bendi ya Njenje, John Kitime na Meneja wa bendi ya Mapacha watatu, Khalid Chokoraa.

LEO MCHANA

Image
Mchana huu wajanja wa mjini wanapata menyu safi katika mgahawa wa City Sports Lounge uliopo jengo la kazi eneo la chini ulipokuwa ubalozi wa Uingereza zamani je?,  wewe unapata wapi menyu yako ya mchana huu, hebu jongea City Sports Lounge ujionee na kupata msosi bomba wa mchana lakini pia kwa mpira na burudani ya muziki  ndiyo penyewe kwani kuna luninga saba katika kila eneo la mgahawa huo na kukupa burudani kwa kila mkao utakaokaa. Hii ndiyo Mandhali ya City Sports Lounge mchana huu kama inavyoonekana watu wakijipatia menyu yao ya mchana.

KAIMU MKURUGENZI MPYA WA ATCL

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Shirika la Ndege la Air Tanzania (ATCL), Kapteni Milton Lusajo Lazaro. Na mwandishi wetu  IKIWA siku mmoja tu baada ya kuteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Shirika la Ndege la Air Tanzania (ATCL), Kapteni Milton Lusajo Lazaro amesema shirika hilo linanafasi kubwa ya kupata mafanikio iwapo litaendelea kutekeleza mpango wake wamaendeleo wa miaka mitano. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana, Lusajo alisema atatumia uzoefu wake alioupata katika sekta ya usafiri wa anga kuleta mabadiriko katika shirika hilo na kuliwezesha kushindana sambamba na kampuni nyingine za ndani na nje ya nchi. Kpt. Lusajo rubani anaeheshimika katika sekta ya usafiri wa anga si kwa Afrika Mashariki pekee ila Afrika kwa ujumla na anarekodi ya kuendesha ndege kwa masaa zaidi ya elfu kumi na mbili na pia amewahi kushika nyadhifa tofauti katika Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) pamoja na ATCL kabla ya kuteuliwa kuwa Kaimu Mk

KCB YAZINDUA HUDUMA MPYA

Image
Mwenyekiti mtendaji wa benki ya KCB Tanzania dk.Edmund Mndolwa katika hafla ya uzinduzi wa KCB DIASPORA BANKING iliyo fanyika leo Dar es salaam