Posts

Showing posts from July 25, 2012

SERIKALI IMESEMA HAIJADHULUMU MALIPO YA WAHANGA

Image
SERIKALI imesema kuwa hakuna malipo  ya kiasi  kidogo cha fedha kilicholipwa kwa waathirika wa mlipuko wa  mabomu ya  Kambi ya jeshi  ya  Mbagala  yaliyotokea mwaka 2009 kama ilivyoripotiwa na gazeti moja la kila wiki la hapa nchini hivi karibuni. Akizungumza na Idara ya Habari( MAELEZO) jana ofisi kwake , Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick alisema hakuna fidia ya Shs. 1400  na Shs. 2500 iliyotolewa kuwa ni ya uharibifu wa jumla ya fidia za malipo kwa wahanga hao, bali malipo hayo ni tofauti ya kiasi cha fedha kilichokuwa  kinadaiwa na wahanga hao ambacho kilichobakia. ‘’ Unajua malipo ya wahanga  hao yalifanyika katika awamu mbili.  Hivyo kiasi cha fedha  cha malipo hayo yaliyotolewa katika hundi hizo , ambayo iliripotiwa katika gazeti hilo ni malipo ya awamu ya tatu.  Malipo hayo ni tofauti ya fedha  kilichokuwa  kinadaiwa na si kweli kuwa wahanga hao walilipwa fedha hizo kama jumla ya fidia za malipo yao,’’ alifafanua Mkuu huyo wa Mkoa.

ILALA IMEJIPANGA VYEMA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO

Image
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akizungumza katika mkutano huo Wajumbe wa mkutano huo wakiwa katika mkutano   Hayo yamesemwa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mhe. Jerry Silaa katika mkutano wa kujenga uelewa kwa viongozi kuhusu program  ya kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto. Akifungua mkutano huo Mhe. Silaa alisema kuwa Manispaa ya Ilala inashiriki kikamilifu katika  utekelezaji wa malengo ya milenia ya kupunguza vifo vya  akina mama na watoto. Alieleza kuwa katika Manispaa ya Ilala kuna vituo mbalimbali vilivyopo katika Hospitali na zahanati kwa ajili ya kupima virusi vya UKIMWI na kuwapatia wathirika wa UKIMWI dawa za kurefusha maisha. Alisema kitu muhimu tunachoijikita nacho hivi sasa ni kupunguza maambukizi ya virusi ya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto. Alisema kuwa Manispaa ya Ilala ina watalaam wa  kutosha wenye uelewa mkubwa wa afya ya Mama na mtoto. ’Ndoto yetu ni ku

SIMBA YAJITETEA.

Image
KOcha mkuu wa Simba Milovan Cirkovic na msemaji wa timu hiyo Ezekiel Kamwaga SIKU moja baada ya kutolewa katika michuano ya Kagame kwa klabu ya Simba, uongozi wa klabu hiyo umewataka mashabiki na wanachama kutulia kwani kikosi hicho ndio kinasukwa.   Makamu Mwenyuekiti wa Simba imu hiyo, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ alisema kikosi cha Simba kinaundwa na wachezaji wengi wageni hivyo bado timu haijawa katika mfumo mmoja.   Alisema hali hiyo ndiyo ilichangia kufanya vibaya kwa timu hiyo katika michuano ya Kagame ambapo Simba ilimalizia mbio zake katika hatua ya robo fainali juzi baada ya kutolewa na Azam Fc kwa mabao 3-1.   “Naomba mashabiki, wanachama na wapenzi wa Simba kuwa watulivu katika kipindi hichi ambacho naamini kuna mengi yatatokea na hasa kwa wale wasioitakia mema timu yetu…napenda ieleweke kwamba kocha yupo katika kupanga kikosi na katika siku zijazo timu itakuwa madhubuti,”alisema Kaburu

Rais Kikwete ashiriki katika mazishi ya mzee Azzan Ally Mangushi

Image
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika mazishi ya kada wa CCM mzee Azzan Ally Mangushi yaliyofanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam jana mchana. Mzee Mangushi aliwahi pia kuwa mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Kinondoni.

NMB YACHANGIA MILIONI 1O/- KWA WAATHIRIKA WA AJALI YA MV SKAGIT

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Kamati ya Maafa Zanzibar, Bw. Ali Juma Hamad (Kushoto), akipokea sehemu ya msaada  kutoka kwa Meneja wa Tawi wa Benki ya NMB Zanzibar, Bw. Mluku Abdallah Maggid, kisiwani Unguja .Msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni 10/- ni maalum kufuatia maafa ya ajali ya MV Skagit iliyotokea Julai 18, mwaka hu u. Maafisa wa Benki ya NMB tawi la Zanzibar wakibeba vifaa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Balozi Ali Seif Idd (Kati), akizungumza na Meneja wa Tawi la Benki ya NMB Zanzibar, Mluku Abdallah Maggid ofisini kwake kisiwani humo wakati akipokea msaada huo. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mhe. Mohammed Aboud Mohammed.
LEO NI SIKU YA MASHUJAA NCHINI TANZANIA

NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME KUFANYIKA KESHO

Image
Nusu fainali zote mbili za kuwania Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) mwaka 2012 zinachezwa kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.   Azam na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) zitacheza nusu fainali ya kwanza kuanzia saa 8 kamili mchana, na kufuatiwa na nusu fainali ya pili kati ya Yanga na APR ya Rwanda itakayoanza saa 10 kamili jioni.