Posts

Showing posts from March 29, 2013

BAADHI ZA PICHA KATIKA TUKIO LA GHOROFA LILILOPOROMOKA ASUBUHI HII YA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

Image
Kamanda wa Kanda maalum ya Kipolisi mkoa wa Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova kulia akizungumza jambo na Mbunge wa kuteuliwa Mh. James Mbatia ambaye ameungana na wananchi wengine katika tukio hilo. Uokoaji ukiendelea katika eneo la tukio. Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadick akiwa katika eneo la tukio kusimamia zoezi la uokoaji. Ulinzi ukiwa umeimarishwa katika eneo la tukio Kibao hiki kinaonyesha kampuni ambazo zilikuwa zikijenga jengo hilo. Kijiko kikiendelea kuondoa kifusi katika eneo la tukio Wananchi wakishiriki katika zoezi la uokoaji kwa kuondoa taka na vifusi katika eneo hilo.

Mbunge wa CUF, Jimbo la Chambani Pemba Salim Hemed Khamis Afariki Dunia,Kuagwa leo, Asubuhi Viwanja Vya Karimjee Jijini Dar es Salaam Kuzikwa Pemba

Image
  Mbunge wa CUF, Jimbo la Chambani Pemba kisiwani Zanzibar, Marehemu,  Salim Hemed    Baadhi ya Maofisa wa Ofisi Ndogo ya Bunge,wakimsaidia kwa kumbeba Mbunge wa Chambani,Bwa.Salim Hemed Khamis,mara baada ya kuanguka ghafla hapo juzi jijini Dar akiwa katika vikao vya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu ya haraka. -- MAZISHI ya aliyekuwa Mbunge wa CUF, Jimbo la Chambani Pemba kisiwani Zanzibar, Marehemu,  Salim Hemed Khamis,yanataraji kufanyika leo mchana mjini Pemba. Taarifa za awali kutoka Chama cha Wananchi CUF, zinasema kuwa Mwili wa Marehemu, Khamis utaagwa leo asubuhi kuanzia majira ya saa 2:30-4:00  katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo Viongozi mbalimbali wa kitaifa na Kimataifa pamoja na wananchi na Wanachama wa CUF watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu. Taarifa hiyo ya Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julis Mtatiro inasema kuwa Msafara

Taarifa Rasmi Kutoka IKULU Kuhusu Ziara ya Rais Jakaya Kikwete Uwanja wa Michezo wa Azam Complex ulioko Chamazi, Temeke, Dar es Salaam unaomilikiwa na Kampuni ya Saidi Bakhressa Group Alhamisi iliyopita, Machi 21, 2013.

Image
 Rais Jakaya Kikwete -- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete  alitembelea na kuzindua rasmi Uwanja wa Michezo wa Azam Complex ulioko Chamazi,  Temeke, Dar es Salaam unaomilikiwa na Kampuni ya Saidi Bakhressa Group Alhamisi  iliyopita, Machi 21, 2013. Rais Kikwete alizindua Uwanja huo wa Azam Complex unaotumiwa na Klabu ya Soka ya Ligi  Kuu ya Tanzania Bara ya Azam FC ikiwa ni tukio la mwisho la ziara yake yenye mafanikio  makubwa ya siku nne katika Mkoa wa Dar Es salaam. Wakati wa hotuba yake ya uzinduzi wa Uwanja huo, Mheshimiwa Rais Kikwete aliipongeza  Klabu ya Azam kwa kuwa dira na mfano nzuri wa  kuendeleza soka nchini na kuwekeza  katika  maendeleo ya mchezo huo unaopendwa na wenye washabiki wengi nchini kwa njia za  kisasa. Tokea siku hiyo ya Alhamisi, Vyombo mbali mbali vya habari nchini yakiwemo magazeti  vimetangaza na kuandika habari nyingi na wachambuzi wa michezo wameandika maoni na