Posts

Showing posts from October 21, 2012

SPIKA WA BUNGE AWASILI CANADA MJINI QUEBEC

Image
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda akiwasili katika uwanja wa ndege mjini Quebec, Canada tayari kwa kuhudhuria mkutano wa 127 wa chama cha Mabunge Duniani (IPU) unaotarajia kufunguliwa rasmi kesho tarehe 21 Oktoba, 2012 na kumalizika 26 Oktoba . Makinda ameongoja ujumbe wa wabunge wanne kutoka Tanzania, ambapo zaidi ya maspika wa nchi 150 duniani wakiongoza ujumbe wa wabunge kutoka Nchi zao watashiriki mkutano huo. Spika wa  Bunge Mhe. Anne Makinda akiteta jambo kuhusu  maandalizi ya awali ya mkutano na afisa kutoka Bunge la Canada mara alipopokelewa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege mjini Canada kuhudhuria mkutano wa 127 wa Chama cha Mabunge Duniani. Kulia ni Mhe. David Kafulila na Mhe. Hamad Rashid waliongozana na Mhe. Spika katika Mkutano huo nchini Canada Mhe. Spika  Anne makinda na ujumbe wake wakionyesha nyaraka muhimu za kusafiria kwa ofisa wa uwanja wa ndege mara baada ya kuwasili kwe nye

FRANCIS CHEKA VS BENJAMIN SIMON NOVEMBER 18, 2012

Image
Mpambano unaosubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa ngumi nchini Tanzania na Ujerumani kati ya Francis Cheka na Benjamin Simon wa Ujerumani sasa utafanyika tarehe 18 November katika ukumbi wa Universal jijini Berlin nchini Ujerumani.    Awali mpambano huo ulikuwa ufanyike tarehe 17 November jijini Berlin, Ujerumani na tayari bondia Francis Cheka ameshasaini mkataba wa kukutana na mbabe huyo wa Ujerumani anayejulikana kwa jina la “Iron Ben” kwa ajili ya ukali wa makonde yanayowasulubu wapinzania wake.     Mtanzania bondia Francs Cheka  Bondia Benjamin Simon ana rekodi ya mapambano 24 ambapo amepoteza pambano moja wakati bondia Francis Cheka ana rekodi ya mapambano 33 amepoteza mapambano 6.   Bondia Benjamin Simon wa Ujerumani   Akimwandikia “Eva Rolle” wa kampuni ya “Primetime Event Management” ya Ujerumani ambaye ndiye promoter wa mpambano huo, mwenyekiti wa ubingwa wa IBF/USBA Lindsey Tucker alimfa

UNIDO YAAHIDI KUONGEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA KATIKA KUKUZA MAENDELEO YA VIWANDA.

Image
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) nchini Tanzania Bw. Emmanuel Kalenzi akifafanua shughuli za Shirika hilo na mafanikio yake hapa nchini ambapo mpaka sasa limeshachagua maeneo yatakayofadhiliwa chini ya ‘Global Environment Facility- GRF’ kwa miradi kadhaa katika mikoa ya Morogoro, Njombe na Rukwa.

YANGA, RUVU SHOOTING YAINGIZA TSH MIL 47/-

Image
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Ya nga na Ruvu Shooting lililochezwa jana (Oktoba 20 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa wenyeji Yanga kushinda mabao 3-2 limeingiza sh. 47,615,000.   Watazamaji 8,233 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyochezwa kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000, na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 8,420,578.47 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 7,263,305.08.   Mgawo mwingine wa mapato hayo ni posho ya msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna wa mechi sh. 203,000, waamuzi sh. 381,000, mwamuzi wa akiba sh. 70,000, usafi na ulinzi wa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (stadium technical support) sh. 2,000,000.   Umeme sh. 300,000, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000, ulinzi wa mechi sh. 3,500,000 wakati tiketi ni sh. 2,959,100. Gharama za mchezo sh. 2,806,859.49, uwanja sh. 2,806,859.49, Kamati ya Ligi sh. 2,80

MARY CHIZI AIBUKA KIDEDEA KWENYE MASHINDANO YA MICHEZO MBALI MBALI

Image
  Mshiriki wa Redd's Miss Tanzania 2012,Mary Chizi ndie alieibuka kidedea leo katika mashindano ya Michezo mbali mbali iliyowashirikisha wa rembo wote wa Redd's Miss Tanzania 2012 , ambapo yeye ameweza kuwa kinara katika michezo mitatu mf u lulizo u kiwemo wa kuogelea na kuwaacha wenzake wakijikongoja.Mary Chi zi anaungana na wenzake wawili wa lioshinda mataji ya Miss Ph oto genic (Lucy Step han) na Top Model (Magdalen a Roy) amba o kwa pamoja wataingia moja kwa moja kat ika hatua ya nusu fainali ya Redd's Miss Tanzania 2012 mwaka huu.  Warembo walioingia hatua ya Tano Bora katika mashindano ya Michez o Mbali m bali wakiwa kwenye picha ya pamoja.  Warembo wa tatu walio jihakikishia ku ingia hatua ya nusu fainali ya Mashindano ya Redd's Miss Tanzania 2012 .Kutok a kulia ni Lu cy Stephan (Redd's Miss Photogenic),Mary Chizi (Redd's Miss Tanzania Sports Lady) pamoja na Magda lena Roy (Redd's M iss Tanzania T op Model).  M kurugenzi

YANGA YAIFUNGA RUVU SHOOTING MAGOLI 3-2 UWANJA WA TAIFA JANA

Image

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO MKUU WA NANE WA JUMUIYA YA UMOJA WA WANAWAKE TANZANIA (UWT) MJINI DODOMA JANA

Image
VURUGU PIA ZILITOKEA KATI YA SHY-ROSW-BANJI NA WAFUAS WA MH. SOPHIA SIMBA Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa akifungua mkutano Mkuu wa nane wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) uliofanyika leo Oktoba 20, 2012 katika ukumbi wa Chuo cha Mipango, mjini Dodoma, sambamba na uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Taifa. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye Ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma leo Oktoba 20, 2012 kwa ajili ya kufungua mkutano Mkuu wa nane wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) uliofanyika sambamba na uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Taifa. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT waliohudhuria mkutano huo leo katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma. Picha na OMR Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,