Posts

Showing posts from May 31, 2012

SERIKALI ITALINDA AMANI KWA NGUVU ZAKE ZOTE

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein ,alipokuwa akizungumza na Wahariri na Waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali vya Bara na Visiwani,katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] Na Juma Mohammed, MAELEZO  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein amesema kwamba Serikali italinda amani kwa nguvu zote na kuonya kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua watakaochochea na kufanya vurugu.   Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Ikulu Zanzibar jana,Dk. Shein alisema “Tutailinda amani kwa nguvu zote, atakayethubutu kuchezea tutamshughulikia kwa mujibu wa sheria”  Rais Shein alisema amesikitishwa sana na vitendo vilivyotokea wiki iliyopita na kuelezea vurugu hizo zimeharibu sifa njema ya Zanzibar ambayo kwa miaka mingi ianjulikana kwa uvumilivu wa kidini kiasi cha hata Serikali ya kikoloni mwaka 1953 kuamua kufanya shindano la uchoraji wa st

OKWI KUUZWA SIMBA KWA SH. BILIONI 2

Image
UONGOZI  wa Klabu ya Simba umewataka baadhi ya watu kuacha tabia ya kutaka kutangaza kuwa wanamchukua mchezaji Emmanuel Okwi wakati wakijua ni mchezaji halali wa  klabu hiyo. Ofisa habari wa Simba Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa  kuna baadhi ya watu wameanza kutumia jina la Okwi kama njia ya kupata uongozi au  kuonekana bora katika klabu zao huku zikiwa hazijawahi hata siku moja kufanya maongezi na k labu ya Simba. Alisema kama kuna klabu inataka kumsajili mchezaji huyo ifuate utaratibu wa kuongea na  viongozi wake kwa kuwa mchezaji huyo bado ni mali ya Simba. Aliongeza kuwa kama kuna mtu au klabu inataka imsajili Okwi inatakiwa kutumia zaidi ya  bilioni 2 ili iweze kumchukua. Alisema mchezaji huyo anatakiwa katika mabala ya ulaya kama Tanzania kuna mtu  anauwezo wa kutoa fedha hiyo klabu ya Simba ipo tayari kumuuza kwa pesa hiyo. "Tupo tayari kumuuza kama kuna klabu hapa nchini ina bilioni 2, sisi tunamuachia kwa kuwa bado mchezaji wetu na anaendelea kuitumikia klabu yetu

WANAFUNZI WAKISHIKIRIA MABANGO KUONESHA WANAPINGA UVUTAJI WA SIGARA

Image
Wanafunzi wakimkimbilia  mzungu kumuonesha mabango yanayokataza kuvuta tumbaku wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kukataza kuvuta Tumbaku Duniani leo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa jULIUS nYERERE, Dar es Salaam. Wakiendelea kumuandama mzungu huyo ambaye hata aliendelea kuvuta sigara bila hofu Mzungu akiwa amezingirwa na matango kila mahala Hatimaye ameamua kusalimu amri na kuanza kusoma tangazo                                         ASkiwa hoi baada ya purukushani hiyo. PICHA NA KHAMIS MUSSA

RAIS SHEIN AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI

Image
Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali vya Zanzibar na Tanzania Ikulu Zanzibar.   Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad,na Mawaziri wakimsikiliza Rais wa Zanzibar Dk. AliMohamed Shein akizungumza na Waandishi Ikulu Zanzibar.   Mawaziri wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari Ikulu Zanzibar   Wahariri wa Vyombo vya Habari na Waandishi wa Habari wakimsikiliza Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, akizungumza na Waandishi Ikulu Zanzibar.   Mwandishi  habari Salim Said  akiuliza swali kwa Rais wa Zanzibar wakati wa Mkutano na Waandishi Ikulu Zanzibr leo.   Mdau wa habari Farouk Karim akiuliza swali wakati wa Mkutano na Waandishi na Rais wa Zanzibar.   Mwandishi Mwantanga Ame alipata fursa ya kuuliza suwali katika Mkutano  wa Waandishi na Rais wa Zanzibar.   Mhariri Manyerere akiuliza suali kwa Rais wa Zaziba
Image
Wachezaji wa Brazil wakilinda ngome yao kwa kuwadhibiti timu ya US kwenye mechi hiyo ya kirafiki ambapo timu ya Brazil waliweza kuwabamiza US bao 4-1 nyumbani kwao. US. hoi kwa Brazil baada ya kubamizwa bao nne bao la kwanza lilifungwa na Neymar, na lapili na Thiago mnamo wa dakika ya 11, kipindi cha kwanza. bao la US lilifungwa na Hercules Gomes dakika ya 44 kipindi chakwanza hadi mapumziko Brazil 2 US 1 kwenye mchezo wa kirafiki. (Picha maelezo na swahilivilla.blog spot.com) Forward wa United States Landon Donovan, akipandisha majeshi juu huku alidhibitiwa na Brazil defender Marcelo wa Brazi katika mpambano wa kirafiki. Hivyo ndivyo ilivyo katika uwanja wa FedexFeild, uliopo Landover Maryland Nchini Marekani
Image
Image
Image

WABUNGE WAKIANGALIA MPIRA HUKO MAREKANI

Image
Waheshimiwa Nassari na Mchungaji Msigwa

JK AFUNGUA MKUTANO LEO ARUSHA

Image
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano wa Mkuu wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Africa afDB katika ukumbi wa AICC jijini Arusha leo Mei 31. 2012.   Rais Kikwete akiwa na Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara, Rais Mstaafu wa Botswana Mh Festus Moghae, Rais wa Benki ya Africa Dkt Donald Kaberuka, Mshauri wa Mfalme wa Morroco Bw Omar Kabbaj (kushoto) , Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa (wa pili kuhsoto) muda mfupi kabla ya kuzindua mkutano Mkuu wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Afruka katika ukumbi wa AICC jijini Arusha leo Mei 31, 2012.PICHA/UKULU

MAKAMU WA RAIS BILALI NA MAKAMU WA RAIS WA IRANI WASAINI MKATABA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, na Makamu wa Rais wa Kwanza wa Iran, Mhe. Mohammad Reza Rahimi, wakibadilishana mkataba baada ya kusaini mkataba huo wa makubaliano ya pamoja ya masuala mbalimbali yanayohusu uhusiano wa nchi hizo mbili,  wakati wa hafla hiyo fupi iliyofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam jana Mei 30, 2012. Picha na Amour Nassor-OMR

MAUAJI RUVUMA

Image
Jeshi la polisi mkoani Ruvuma limewatia mbaroni watu wawili wakazi wa eneo la Mkuzo katika halmashauri ya manispaa ya Songea ambao wana uhusiahano wa kimapenzi kwa tuhuma za kumuua mtoto mdogo wa jinsia ya kike mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi mitatu  kwa madai kuwa mtoto huyo amekuwa akikwakosesha starehe zao za kimapenzi pale wanapohitaji kukutana. Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Michael Kamhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa mbili na nusu asubuhi huko katika eneo la Mkuzo ambako inadaiwa kuwa mtoto huyo aliuwawa kwa kunyongwa shingo na watuhumiwa ambao aliwataja kuwa ni Jema Msemwa (19) na Yohana Njelekela (22) wote wakazi wa Mkuzo. Alifafanua kuwa inadaiwa kuwa Mei 29 mwaka huu majira ya saa za asubuhi huko katika kituo cha polisi cha mjini Songea ilipokelewa taarifa kuwa kuna binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Jema mkazi wa Mkuzo ambaye alikuwa na mtoto mdogo wa kike aitwae Rebeca Cheni (1.3) alikuwa amefika ny

MAIGE AKUMBWA NA MKASA MWINGINE

Image
Mapema wiki hii Mbunge wetu wa jimbo la Msalala, Mh. Ezekiel Maige alitoa shutuma dhidi ya Vikao vya juu vya chama hasa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kuwa havikumuita kumhoji juu ya  tuhuma zinazomkabili.         Lakini pili alitoa shutuma nzito dhidi ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) , Ndg. Nape Nnauye, kuwa yeye ni gamba namba moja linalotakiwa kuvuliwa, kwa kile kinachodaiwa kutokuwa na mkakati wa kuzuia wanachama wa CCM kuhamia vyama vya upinzani na kuingiza wanachama wapya.        Mh. Maige anadai Nape kashindwa kubuni mbinu za kuingiza wanachama na zaidi kupambana na wimbi la kuhama kwa viongozi, makada na wanachama wa CCM.        Kama katibu Mwenezi wa CCM Wilayani Kahama kwa kutambua umuhimu wa vikao, na kwa kuheshimu mamlaka ya kikatiba ndani ya Chama, nimeona si vema kukaa kimya bila Kutolea ufafanuzi tuhuma hizo ambazo kwa ujumla zinalenga kukivuruga na kukichafua Chama chetu.          Chama chetu kinao utar

TAIFA STARS WAONDOKA ALFAJIRI YA LEO

Image