Arsenal tayari kununua hisa zaidi


Alisher Usmanov
Alisher Usmanov

Tajiri mmoja anayemiliki kiasi kikubwa katika hisa za klabu ya Arsenal, Alisher Usmanov anasema angependa kununua hisa zaidi za klabu hio ingawa hana nia ya kupata nafasi kwenye bodi inayoongoza klabu.
Usmanov ambaye ndiye tajiri mwenye vipesa kuliko tajiri mwingine nchini jimbo la zamani la Urussi la Uzbekistan, ni mmoja wa matajiri kadhaa wanaomiliki hisa katika klabu za Uingereza kama Roman Abramovich huko Chelsea na Anton Zingarevich wa Reading.
Arsenal fc
Arsenal fc
Usmanov ameliambia shirika la habari la Reuters nje ya mji wa Petersburg kua 'daima na kwa kiwango chochote, nipo tayari kuongezea kiwango cha hisa zangu.
Usmanov, ambaye utajiri wake umetokana na biashara ya chuma na teknolojia anaweza kujijengea umaarufu na nafasi kwenye bodi kutokana na kiwango cha hisa atakazowekeza.
Chombo cha Red and White, kinachomilikiwa na Usmanov kwa ushirikiano na Farhad Moshiri,wana miliki asili mia 29.72 ya hisa katika Arsenal,kwa mujibu wa Tovuti ya klabu hio.
Stan Kroenke
Stan Kroenke
Licha ya uwezo huo, Usmanov hajioni akiwa kwenye bodi ya viongozi wa Arsenal, na kwa kauli yake anasema 'singependa kuhudhuria mkutano wa bodi bila kualikwa.
Kwa mujibu wa habari za vyombo vya habari mmiliki mkubwa wa hisa za Arsenal, Kroenke anachukizwa kusikia kama Usmanov angepewa nafasi kwenye bodi ya Arsenal.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA