Lowassa avipiga jeki vikundi saba vya vikoba Monduli mjini
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa
amevipatia vukundi saba vya Vikoba vilivyopo Wilayani Monduli,kiasi cha
shilingi milioni nane kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao.Lowassa
amesema yeye ni mkereketwa mkubwa wa Vikoba huku akisisitiza kuwa ni
chachu ya maendeleo na kumkwamua mtanzania kutoka katika umasikini. kila
kikundi kimepata shilingi millioni moja ambapo kikundi kilichofanya
vizuri kimeongezewa shilingi millioni moja zaidi.Pichani ni Mh. Lowassa
akikabidhiwa zawadi na mwenyekiti wa Vikoba Kijiji cha Monduli
Juu,Dawson Kaaya wakati viongozi wa vikundi hivyo walipomtembelea
nyumbani kwake Monduli.
Mmoja wa viongozi wa vikundi vya vikoba Kijiji cha Monduli Mjini akisoma risala mbele ya Mh Lowassa.
Baadhi ya wanavikoba wa Monduli Mjini wakimsikiliza Mh. Lowassa.
Mhe
Edward Lowassa akipewa zawadi na Bi Arafa Ismaild kutoka katika vikundi
vya Vikoba Monduli mjini ambao walikwenda kumtembelea nyumbani kwake.
Kushoto kwa Mhe ni Bw. Dawson Kaaya ambaye ni Mwenyekiti wa Vikoba
Monduli Mjini