WAZIRI MKUU MSTAAFU AWASHAURI WABUNGE KUANZISHA SHULE
Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa (wa pili kushoto) akijumuika pamoja na Baadhi ya Wabunge wanaounda timu ya Bunge Sports inayoundwa na wabunge kutoka Baraza la Wawakilishi na Bunge la Jamhuri, wakati wa Chakula cha Mchana alichowaandalia Nyumbani kwake, Ngarashi Wilayani Monduli. Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo,Amos Makalla, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Iddi Azzan pamoja na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Monduli, Reuben ole Kunai.
WAZIRI Mkuu mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward
Lowassa amewashauri wabunge wa timu ya Bunge Sports kufikiri juu ya
kutunga sera ya michezo itakayoruhusu kuanzishwa kwa Shule za Michezo
(Sports Academy) hapa nchini. Lowassa ameyasema hayo jana, baada ya
kuialika nyumbani kwake timu hiyo iliyopiga kambi ya jijini Arusha
tayari kwa mashindano ya Mabunge ya Afrika Mashariki jijini Nairobi.
“Nilisikitika kweli Timu ya Taifa ya Kilimanjaro Stars ilipofungwa na
Burundi kwenye mchezo wa pili wa Mashindano ya CECAFA huni Uganda,
pamoja na juhudi za Rais Jakaya Kikwete kuleta makocha bado tumefungwa
na Burundi iliyotoka kwenye vita juzi!.
“Nyinyi ni watunga Sera, ni wachezaji mnajua changamoto zinazofanya
tusifike juu, umefika wakati wa kuwa na Shule za Michezo zinazotambuliwa
na Sera zetu.
“Mpira ni chakula cha Watanzania, wanapenda mpira sana. Napendekeza
baada ya kurejea anzeni kufikiria juu ya kutunga Sera ya kuwa na Shule
za Michezo. Kipingu amejitahidi kuwa na kitu kama hiki lakini amebakia
peke yake hakuna anayemuunga mkono,” alisema Lowassa.
Alisema
kuwapo kwa Timu ya Bunge Sports kutasaidia kufikiria juu ya
mafanikio ya mchezo wa mpira wa miguu, pete na michezo mingine. Kwa
upande wake Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos
Makalla aliyeongozana na timu hiyo alimwambia Lowassa kwamba serikali
ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha Sera za michezo.“Sera na
sheria za sasa za michezo kweli haziendani kabisa na wakat,zote ni za
zamani. Serikali imejipanga kuzifanyia kazi.
“Changamoto uliyoitoa ya kuanzisha Shule za Michezo na kuendeleza michezo nchini tunaipokea na tutaifanyia kazi.
“Nilipoteuliwa
kuwa Naibu Waziri kwenye Wizara hii niliwaambia watu
na binafsi namshukuru Rais Kikwete, kwamba upele ulipata mkunaji kwani
mimi ni mwanamichezo na uwanjani ni kiungo mchezeshaji,” alisema
Makala.Naye Mwenyekiti wa Timu hiyo ya Bunge Sports inayoundwa na
wabunge
kutoka Baraza la Wawakilishi na Bunge la Jamhuri, Iddi Azan alimshukuru
Mh. Lowassa kwa mawazo yake na kuahidi kuyafanyia kazi.
“Kwanza tunaahidi ushindi kwa nchi, Bunge letu na haya uliyoyasema
tunaahidi kuendelea kuyafanyia kazi kwani tunatambua sheria na Sera za
michezo zimepitwa na wakati,” alisema Azan.
Timu hiyo ya Bunge Sports ilikuwa na wachezaji wake wote waliopo
kwenye kambi jijini Arusha wanaounda timu ya Mpira wa miguu na Pete