UJUMBE WA BODI YA KIMATAIFA YA PLAN INTERNATIONAL WATEMBELEA MIRADI YA SHIRIKA HILO IKIWEMO KITUO CHA WATOTO CHA MLEGELE-KISARAWE.
Wakazi wa Wilaya ya Kisarawe wakicheza ngoma ya kiutamaduni pamoja na
mmoja wa wajumbe wa bodi ya Plan International waliotembelea moja ya
miradi inayofadhiliwa na shirika hilo wilayani humo.
Mlezi
wa Kituo cha Mlegele Wilayani Kisarawe na Mwenyekiti wa Majengo yote ya
Kulelea watoto hao Bw. Shabani Daruweshi akisoma risala kwa ujumbe wa
Bodi ya Plan International (haupo pichani) ambapo amesema Shirika la
Plan International limeshirikiana kikamilifu na Wanajamii, Serikali na
Mashirika mengine katika kufadhili taratibu zote za kuwajengea uwezo wa
kitaalam wadau mbalimbali, akitolea mfano kuijengea uwezo wa kitaalam
timu ya Wilaya ya wataalam wa malezi na makuzi ya mtoto katika wilaya ya
Kisarawe.
Amesema
pamoja na mafanikio waliyoyapata bado wankabiliana na changamoto kadhaa
ikiwemo Miundo Mbinu ya kituo kutokuwa rafiki wa watoto ikiwa ni pamoja
na majengo ya kudumu, uhaba wa maji safi na salama, upungufu wa vyumba
vinne vya madarasa kwa ajili ya shule ya msingi, nyumba ya walimu,
ofisi, kituo cha afya ili kupunguza umbali wakupata elimu ya msingi kwa
wakazi wa Mlegele.
Mlezi
wa Kituo cha Mlegele Wilayani Kisarawe na Mwenyekiti wa Majengo yote ya
Kulelea watoto hao Bw. Shabani Daruweshi akikabidhi risala kwa ujumbe
wa bodi ya kimataifa ya Plan International ambao umesheheni changamoto
kadhaa zinazohitaji kutatuliwa.
Ujumbe wa Bodi ya Kimataifa ya Plan International uliotembelea Kituo cha
watoto cha Mlegele kilichopo wilayani Kisarawe mkoani Pwani.
Baadhi ya Wakazi wa Kisarawe mkoani Pwani wakisiliza yaliyokuwa yakizungumzwa na Ujumbe wa Kimataifa kutoka Plan International.
Mkufunzi wa Wauguzi Bi. Maseif Mchachura akitoa chanjo kwa mmoja wa
watoto eneo la Mlegele Wilayani Kisarawe wakati Ujumbe wa bodi ya Plan
International ulipotembelea eneo hilo na kukagua miradi inayofadhiliwa
na shirika hilo.
Gari la kutoa huduma za mbalimbali za tiba lililotolewa na Daichi Sankyo
kupitia shirika la Plan International linalotoa huduma kwa jamii ya
Wakazi wa Mlegele wanaoishi wilayani Kisarawe mkoani Pwani ambapo
huzunguka kuwasaidia watoto wachanga wanaozaliwa hadi wamama wajawazito
na wengineo.
Mfanyakazi
wa Plan International kutoka nchini Kenya Grace Ndungu akichukua
maelezo kutoka kwa Mkufunzi wa Wauguzi Bi. Maseif Mchachura annayetoa
huduma katika Mobile Clinic iliyopo Wilayani Kisarawe kwa niaba ya Plan
International.
Mkufunzi
wa Wauguzi Bi. Maseif Mchachura wa Mlegele Wilayani Kisarawe akionyesha
ujumbe wa Bodi ya Plan International dawa wanazotumia kusaidia kinamama
pamoja na watoto wanaogua hata watu wazima wanaopata Malaria na
magonjwa mengineo.
Ujumbe wa Bodi ya Plan International ukizungumza na watoto wa shule ya
awali ya kituo cha Watoto cha Mlegele ambacho kimedhaminiwa na shirika
hilo kuhakikisha watoto wenye umri wa kuanza shule wanaweza kupata elimu
hiyo.
Mmoja wa watoto wa shule ya Awali ya Mlegele akipata kikombe cha uji.
Mmoja wa wafanyakazi wa Plan International Tanzania akionyesha jiko
linalotumiwa kupika uji kwa ajili ya watoto wa shule hiyo ya awali kwa
ujumbe wa bodi ya Plan International iliyotembelea kituoni hapo kukagua
miradi inayofadhiliwa na Plan International.
Kichanja cha kuanikia vyombo vinavyotumiwa na watoto wa kituo cha Mlegele kunywea uji.
Baadhi
ya watoto wa shule ya msingi katika kituo cha watoto cha Mlegele wakati
wa ziara ya ujumbe wa bodi ya Plan International ulifika Kisarawe
kukagua miradi ya Shirika hilo.