BENKI YA NBC WATOA ZAWADI ZA X-MAS NA MWAKA MPYA
Baadhi wa watoto wanaolelewa katika kituo cha CHAKUWAMA, Sinza jijini Dar es Salaam wakionyesha baadhi ya vitu walivyopewa kama msaada na wafanyakazi wa Benki ya NBC kituoni hapo juzi ikiwa ni sehemu yashamrashamra za Sikukuu za Christmas na mwaka mpya. .
Meneja Mwandamizi Idara ya Utendaji wa Benki ya NBC, Salim Rupia (kulia) akikabidhi msaada vyakula na vitu vingine vilivyotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo kwa Katibu wa kituo cha kulelea watotoyatima cha CHAKUWAMA, ndugu Ally Saidi kituoni hapo, Sinza, Dar es Salaamjuzi ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za Sikukuu za Christmas na mwakampya.
Meneja Huduma kwa Wafanyakazi wa NBC, Suzyo Gwege-Nyirenda (kulia) akikabidhi msaada vyakula na vitu vingine kwa watoto wanaolelewakatika kituo cha CHAKUWAMA, Sinza jijini Dar es Salaam vilivyotolewana wafanyakazi wa benki hiyo ikiwa ni sehemu ya shamrashamra zaSikukuu za Christmas na mwaka mpya. Wafanyakazi hao walichanga zaidi ya shs milioni 3 kwa ajili ya vitu hivyo na sehemu ya pesa itatumika kulipia ada za shule kwa baadhi ya watoto mwakani.