ZIARA YA MKUU WA MKOA WA RUKWA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiongea kwa ukali wakati akionyeshwa ramani na Mpima wa Manispaa Selice Nzyungu ya eneo alilouziwa muwekezaji Ephatta Ministry na lile walilopewa wananchi wa kata ya Mollo katika Manispaa ya Sumbawanga. Mkuu huyo wa Mkoa amelazimika kutembelea eneo hilo baada ya kupewa taarifa za awali na Kamati aliyoiunda katika kufuatilia mgogoro unaoendelea kati ya muwekezaji na wananchi wanaolizunguka shamba hilo. Lengo kuu la ziara yake hiyo ya tarehe 02, Septemba 2012 ilikuwa ni kutembelea mashamba yakiwemo ya muwekezaji na wananchi pamoja na kuzungumza na wananchi na muwekezaji kwa kuchukua kero zao kwa ajili ya kuutafutia ufumbuzi mgogoro huo. 

Mkuu huyo wa Mkoa wa Rukwa akizungumza kwenye Mkutano na wananchi wa kata ya Molo ambapo pia wawakilishi wa muwekezaji walialikwa kuskiliza na kutoa kero zao mbele ya wananchi wa kata hiyo. Hata hivyo baada ya Mkuu huyo wa Mkoa kusikiliza kero hizo aliwaahidi wananchi pamoja na muwekezaji kuendelea kuushughulikia Mgogoro huo kuanzia ngazi ya Kijiji, Kata, Wilaya, Mkoa, Wizara na Taifani kwa ujumla kwa ustawi wa wote na maendeleo ya Mkoa na Nchi kwa ujumla. Alisema kuwa lengo lake sio kuegemea upande mmoja bali ni kutafuta haki kwa kila pande. Aliwataka wananchi na muwekezaji kufungua upya milango ya mahusiano mazuri baina yao ili kumuunga mkono katika kutafuta suluhu ya mgogoro huo ambao umekuwa ukiibua sura mpya kwa vipindi tofauti.
Wananchi wakitoa kero zao mbalimbali zikiwepo unyanyaswaji kwa kuchapwa viboko na kukatwa maskio kwa pindi wakutwapo na muwekezaji huyo wakipita shambani kwake au wakikata nyasi kwa ajili ya kulishia mifugo yao. Kero nyingine waliyoitoa ni kukosa maeneo ya kulima na kupata kipato kutokana na eneo kubwa kupewa muwekezaji ambalo eneo alilopewa ni hekta alfu kumi (10,000) kwa ajili ya ufugaji kwa mujibu wa Mkataba. Uharibifu wa barabara pamoja Muwekezaji huyo kwenda kinyume na Mkataba wake wa kufuga na badala kulima zaidi ni kero pia ambayo waliitoa wananchi hao wa kata ya Molo.
Ndugu Josephat Mutarabuga ambaye ni muwakilishi na mfanyakazi wa Ephata Ministry Heritage Pharm linalomiliwa na Ephata Minisrty akitoa kero za muwekezaji huyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ambazo ni uharibifu wa wananchi kwenye shamba lao. Alisema kuwa wananchi wa Vijiji vya mawenzusi wamekuwa wakichoma moto mashamba yao hali inayopelekea uharibifu mkubwa wa mazao yao. Alisema pia kuwa wananchi wa vijiji hivyo hukata pia mazao ya mahindi ambayo bado ni mabichi kula Migagi (Kula mashina ya Mahindi kama miwa)

Sehemu ya wananchi, viongozi wa serikali na wawakilishi wa muwekezaji wakiwa kwenye Mkutano huo uliofanyika tarehe 02, Septemba 2012.

Wawakilishi wa Ephata Ministry wakitambulishwa kwenye Mkutano huo. (Picha na Hamza Temba-Rukwareview.blogspot.com-Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA