MAANDALIZI YA MKUTANO




Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Theresia Huvisa akizungumza na wandishi wa habari jijini Arusha leo kuhusiana na maandalizi ya mkutano wa 14 wa Mawaziri wa Mazingira kutoka barani Afrika Tanzania ikiwa mwenyeji wa mkutano huo.
 
Na.MO BLOG -Arusha
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) nchini Tanzania Mh. Theresia Huviza anatarajiwa kutangazwa rasmi kuwa Rais wa Mazingira kwa Afrika katika Mkutano wa 14 wa Mawaziri wa mazingira unaofanyika Arusha nchini Tanzania kuanzia kesho hadi tarehe 14 mwezi huu.
 
Waziri Huviza ataongoza kwa kipindi cha muda wa miaka miwili ambapo baada ya hapo nafasi hiyo itachukuliwa na nchini nyingine. Mkutano huo umefanikishwa na European Union, Ubalozi wa Norway, Global Environmental Facility, UNEP na UNDP na wajibu mwingine ukifadhiliwa na serikali yenyewe.
 
Bajeti ya maandilizi ya mkutano huo imegharimu takriban dola za kimarekani 350,000 sawa na shilingi za Tanzania zaidi ya milioni mia 6.
Pichani juu na chini ni Watoto wakifanya mazoezi ya wimbo maalum watakaoimba kesho kwenye mkutano wa 14 wa mawaziri wa mazingira barani Afrika mbele ya Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) nchini Tanzania Mh. Theresia Huviza.
Harriet Macha kutoka Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa(kushoto) akitoa maelezo mmoja wa wadau wa mazingira aliyefika katika banda la Umoja wa Mataifa lililopo katika jengo la AICC utakapofanyika mkutano wa 14 wa mawaziri wa Mazingira.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu aktioa maelezo kwa mmoja wa wadau ya namna Umoja wa Mataifa inavyoshirikiana na Serikali ya Tanzania katika utunzaji wa Mazingira kupitia mpango wa mazingira (UNEP) uliopo chini ya Umoja wa Mataifa.
Banda la ROA OZONE ACTION PROGRAMME chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais na UNEP wakitoa maelezo katika kutunzaji wa mazingira kwa wananchi

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA