UZINDUZI WA JALIDA LA ILALA


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (katikati) akizungumza wakati alipozindua jarida la ‘SAUTI YA ILALA’ ambapo amesema kwa sasa halmashauri hiyo inajiendesha kisasa sana, wanakusudia kuwa na jarida ambalo kweli litafanya kazi ya kuitangaza Ilala, na kufikisha ujumbe si tu kwa wananchi wa Ilala bali kwa Jamii nzima.
Aidha amewataka wafanyabiashara wa Ilala kujitangaza katika gazeti hilo ili fedha zitakazopatikana sio tu zitalipia gharama za uchapishaji bali fedha zitakazobakia zitatumika kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii. Kulia ni  Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Paul Wanga na Kushoto ni Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala Tabu Shaibu, Mkurugenzi wa Kampuni 361 Mustafa Hassanali, Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Kheri Kessy.
Wageni waalikwa wakipitia toleo la zamani la Jarida la Sauti ya Ilala kabla ya uzinduzi rasmi.
Pichani Juu na Chini ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (wa tatu kulia) na Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Kheri Kessy wakifungua pazia kuashiria uzinduzi rasmi wa ‘Jarida la Sauti ya Ilala’.  Wanaoshuhudia tukio hilo Kulia ni Mh.Sada Madwangwa, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Paul Wango na kushoto ni Mkurugenzi  wa Kampuni ya 361 Mustafa Hassanali ambao ndio waandaaji wa uzinduzi huo.
Sasa limezinduliwa rasmi.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (katikati), Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Kheri Kessy (wa pili kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa wakikata keki yenye mfano wa jarida hilo  kwa pamoja mwendelezo wa uzinduzi wa Jarida hilo.
Wageni waalikwa wakisoma jarida hilo.
Baadhi ya Waandishi wa habari wakipitia jarida hilo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (kulia) akipata picha ya ukumbusho na Mmoja wa wadhamini wa jarida la Sauti ya Ilala Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd. Bw. Imran Karmali (katikati).
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akimshukuru mmoja wa wadhamini wa Jarida hilo Meneja Masoko na Afisa Uhusiano wa Benki ya Exim Linda Chiza.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA