UWAMADAMUDA



 
UMOJA wa Wamiliki wa Maduka ya Dawa Muhimu Dar es salaam (Uwamadamuda), umesema pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kusitisha zoezi la Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA),  bado unaitaka  serikali kutafuta suluhu ya kudumu.
Hatua hiyo imekuja baada muongozo mpya wa TFDA unaowataka  wamiliki hao wa maduka ya dawa kuhamia  pembezoni mwa jijji Dar es Salaam.
 
Akizungumza na wandishi wa habari jijini jana, Makamu Mwenyekiti wa Umoja huo, Juma Maganga, alisema waziri anapaswa kutoa suluhu ya kudumu na siyo kwa muda kama alivyoagiza, ili wamiliki hao wafanye biashara zao kwa amani.
 
“Kwa kuwa serikali yetu ni sikivu na inajali raia wake hivyo tunamsisitiza Waziri , Hussein Mwinyi kuwa tunategemea suluhu ya kudumu atakayotoa itaondoa ubaguzi na ukandamizaji kwa wenye mitaji midogo”alisema Maganga
 
Maganga alisema iwapo Wizara itashindwa kutoa uwamuzi wa kudumu kuhusu muongozo huo kuna hatari mvutano ukaendelea na hatimaye kufikishana kwenye vyombo vya sheri

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA