RAIS KIKWETE AKAGUA GHALA LAKE LA MAHINDI MSOGA LEO
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na mjukuu wao
Aziza Ridhiwani (3) katika ghala ya mahindi yaliyovunwa kwenye shamba
lao kijijini Msoga, nje kidogo ya mji mdogo wa Chalinze, Mkoa wa Pwani.
Rais Kikwete ni mkulima na mfugaji kijijini hapo na ameonesha
kufurahishwa sana na mavuno makubwa ya mahindi shambani kwake. Hii
katika kutekeleza kwa vitendo sera ya Serikali ya kuendeleza kwa ari
mpya, kasi mpya na nguvu mpya sekta ya kilimo katika Tanzania.