KIGODAAITAKA TBS KUFANYA UKAGUZI



WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda amelitaka Shirika la Viwango (TBS), kuhakikisha linafanya ukaguzi wa bidhaa kutoka nje kabla hazijaingizwa nchini ili kuepukana na tabia nchi hii kugeuzwa dampo la bidhaa hafifu.
Kauli hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam jana, wakati alipokuwa akizindua Ofisi ndogo ya shirika hilo, inayoshughulika na ukaguzi wa bidhaa zinazotoka nje ya nchi.
Dk Kigoda alisema iwapo shirika hilo litafanikiwa kudhibiti uingizwaji wa bidhaa hafifu nchini anaamini kelele zote zinazopigwa kuwa wao ndio chanzo cha uingizwaji wa biadhaa hizo zitakwisha.
“Nawaagiza TBS kupitia madukani na sokoni ili kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa ubora wa bidhaa na zile bidhaa mtakazokuta ni hafifu, zitoweni na kuziharibu na hao wafanyabishara watozwe faini za kuharibu bidhaa zao”alisema Dk Kigoda.
Alibainisha kuwa Wizara yake inatarajia kupata taarifa juu ya utekelezaji wa maagizo hayo kwa vipindi vya kila robo mwaka ili kujua utaratibu wa utekelezaji.
Akifafanua madhumuni ya wizara ni kushirikiana na taasisi nyingine za serikali kama vile Mamlaka ya Mapato (TRA) Baraza   la Mazingira ,Mamlaka ya Chakula na Madawa (TFDA), Mkemia Mkuu wa  serikali, pamoja na  Tume ya Ushindani  ili kuhakikisha bidhaa za nje zinapimwa maridhawa.
“Ili shehena za bidhaa hafifu zizibitiwe kuingia sokoni na kurudishwa zilikotoka” kwa mujibu Dk Kigoda.
Naye Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi  ya shirika hilo, Oliver Mhaiki   alitabanaisha kwamba uzinduzi wa ofisi hiyo ni muendelezo wa jitihada za shirika kusogeza huduma kwa wateja.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA