KATIBA MPYA


 
 
    
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) kimesema wananchi hawajafungwa kutoa mawazo yao katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba,lakini msimamo wa CCM ni kubaki katika mfumo wa muundo wa Serikali mbili.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Mjini hapa Jana, Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzíbar, Jamal Kassim Ali alisema kimsingi wananchi wako huru kutoa maoni yao kuhusu aina ya mfumo wa Muungano,lakini kwa wanachama wa CCM ni lazima wafuate msimamo wa Chama hicho.

Naibu Katibu Mkuu huyo alisema kwamba Umoja wake unaamini katika kulinda na kuhifadhi umoja na mshikamano uliopo hivyo ni muhimu kwa wananchi kutokubali kushawishiwa kuvunja Muungano.

“Katika suala la Muungano, CCM imeweka wazi kuwa itaendeleza muundo wa Muungano wa Serikali mbili kama inavyoelezwa katika ibara ya 221(a) ya Katiba ya Chama cha Mapinduzi sisi hatuwezi kuikiuka katiba hiyo” Alisema Jamal.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA