WAZIRI FENELLA AFUNGUA MASHINDANO YA UMISETA

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akishuhudia gwaride la maandamano ya wanafunzi wa shule za sekondari wakati wa uzinduzi wa Mashindano ya shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) uliofanyika Kibaha Mkoani Pwani. (Picha na Benjamin Sawe wa WHVUM)


Baadhi ya washiriki wa Mashindano ya shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) wakipita mbele ya mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo,uzinduzi huo ulifanyika jana Mkoani Pwani. (Picha na Benjamin Sawe wa WHVUM)
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akiongea na wachezaji wa Umoja wa Michezo wa shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) (hawapo pichani) wakati alipokwenda kuzindua mashindano hayo Kibaha mkoani Pwani.Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza na Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh.Jumanne Sagini. (Picha na Benjamin Sawe wa WHVUM)
Baadhi ya washiriki wa Mashindano ya michezo mbalimbali ya  shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara wakati wa uzinduzi wa  Mashindano ya shule za Sekondari Tanzania (UMISETA). (Picha na Benjamin Sawe wa WHVUM)

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA