WAZIMBABWE KUCHEZA NA TAIFA STARS NA GAMBIA
Waamuzi
kutoka Zimbabwe ndiyo watakaochezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia
hatua ya makundi Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na
Gambia itakayochezwa Juni 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa
mujibu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) mwamuzi wa
kati atakuwa Ruzive Ruzive. Waamuzi wasaidizi ni Salani Ncube na Edgar
Rumeck wakati mwamuzi wa akiba ni Norman Matemera.
Kamishna
wa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni ni Fanie Wallace Mabuza
kutoka Swaziland wakati mtathmini wa waamuzi (referee assessor) ni Ali
Baligeya Waiswa.
Waamuzi
hao watawasili nchini kesho (Juni 8 mwaka huu) saa 1.20 usiku kwa ndege
ya Kenya Airways wakati Kamishna wa mechi hiyo atawasili siku hiyo hiyo
saa 12.50 jioni kwa ndege ya South African Airways. Mtathmini wa
waamuzi atatua pia Juni 8 mwaka huu saa 7.55 mchana kwa ndege ya Kenya
Airways.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inaendelea na mazoezi
leo saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam chini ya Kocha
Mkuu Kim Poulsen.