SINA MSUGUANO NA WAZIRI


WIZARA ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imekanusha taarifa kuwa kunamsuguano kati ya Waziri na Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.
Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Seth Kamuhanda wakati alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari  jijini Dar es Salaam leo .
Alisema taarifa hizo zilizoandikwa na Jukwaa la wa Hariri Tanzania (TEF),  kwenye vyombo vya habari kuwa hazina ukweli wowote kwani viongozi hao wamekuwa na  ushirikiano mzuri  kati kazi hivyo si rahisi kutokea migongano kama ilivyodaiwa.
Kamuhanda alisema nawaomba wanahabari mkitoka hapa muwafikishiye taarifa hizi wananchi  kuwa katika Wizara hiyo hakuna migongano na wahakikishia kuwa haitatokea kwa kuwa hakuna tofauti yeyote kati yao.
"Unajua hali kama hiyo ya mimi kugongana na waziri kwa kuwa kila mmoja wetu amekuwa akifanya kazi yake kwa uadilifu mkubwa hivyo basi haitatokea hata siku moja kutokea tofauti.
Akizungumzia ni kwa nini walishindwa kufika siku ya kufungua na kufunga mkutano huo alisema taarifa waliyopaswa kujibu na Baraza la Wahariri kutokana na ukweli kwamba waliwafikishia taarifa ya kutofika.
Kamuhanda alisema wakati walipopata mwaliko kipindi hicho Wizara ilikuwa katika maandalizi kuhusu kamati za Bunge jambo ambalo liliwafanya washindwe kuhuria kikao hicho ambapo walifikisha taarifa kwa Watendaji wa jukwaaa.
"Kwa kweli nilishangaa niliposoma hiyo taarifa kwa kuwa tulikwisha zungumza kuhusu kutohudhuria kwetu katika kikao hicho.

Popular posts from this blog

CATHERINE MASUMBIGANA AWA REDD'S MISS CHANG'OMBE

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

HOTUBA YA MHESHIMIWA PEREIRA AME SILIMA (MB), MWENYEKITI WA BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI (T)