PONGEZI KUTOKA KWA MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR


Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi ameipongeza Ofisi ya Tume ya Sayansi na Teknolojia ( COSTECH) na Tume za Nguvu za Atomic (TAEC) kwa uwamuzi wake wa busara  kwa kuamua kufungua ofisi zao hapa Zanzibar
Pongezi hizo alizitoa jana huko Tunguu wakati alipokuwa akizindua Ofisi  hizo alisema kuwa ni faraja kubwa kwa watu wa Zanzibar kupata huduma za Tume ya Sayansi na Teknologia pamoja na Nguvu za Atomic hapa hapa Zanzibar .
Alieleza kuwa tume hizo ambazo zimefungua ofisi zake hapa Zanzibar itasaidia kuwapatia elimu mbali mbali wananchi wa Zanzibar wakiwemo wajasiri amali ambao tayari wameweza kupata elimu ambayo imewafanya kuweza kuuuza bidhaa zilizokamilika.
Aidha akifafanua alisema kuwa bidhaa hizi ambazo zinatengenezwa na wajasili amali zinawafanya waweze kupata  manufaa ambayo  huongeza  harakati ya maendeleo kiuchumi pamoja na kupunguza umasikini nchini.
Balozi huyo alieleza kuwa tume hizi zitasaidia kutoa mchango mkubwa kwa wananchi ikiwemo kuwapa elimu ya tafiti mbali mbali ikiwemo kilimo kuweza kupata mbegu bora , utafiti wa afya ikiwemo maradhi ya saratani ,pamoja na athari ambazo zinapatikana kutokana na mionzi ambayo inaitumiwa na wananchi katika shughuli zetu za kila siku ili kuweza kujua athari hizo na kuweza kuziepuka .
Alifahamisha kuwa shughuli za utafiti zina mchango mkubwa katika kuleta maendeleo ya nchi na umuhimu wake   unaeleweka ambao ni mkombozi wa kuondoa dimbwi la umasikini nchini .
Akifafanua kuwa tume hizo zinategemea kuwashajihisha wasomi mbali mbali kufanya utafiti katika nyanja tofauti kwa manufaa ya nchi.
Nae waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Makame Mbarawa Mnyaa alisema kuwa Tume hizo zitaweka mashirikiano katika masuala ya ICTili kuikuza zaidi chuo kikuu cha Suza ili kuweza kutoa elimu hiyo kwa ufanisi zaidi.
Aidha alieleza kuwa Tume hizo tayari imeshatenga fedha kwa ajili ya kukifanyia matengenezo chuo cha kizimbani pamoja na kufanyia tafiti mbalimbali. 

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA