NAPE AFANYA MAMBO MJI WA SONGEA


Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo kimeiteka Songea, baada ya umati wa wananchi wa mji huo kuhudhuria kwa wingi mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Majimaji. Pichani, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na wananchi baada ya kuwasili kwenye Uwanja huo. (Picha na Bashir Nkoromo)

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM ),Nape Nauye amesema kuwa si sahii kwamba chama hicho kimepoteza mvuto na kukimbiwa na vijana bali hiyo ni propaganda ya uongo na ni vita ya kisaikolojia inayoendeshwa na vyama vya upinzani ambavyo alidai kuwa ni makundi ya wapiga kelele ambayo hayapaswi kupewa madaraka ya kuongoza Nchi.

Alitoa kauli hiyo jana mjini Songea mkoani Ruvuma wakati akiwa kwenye ziara ya siku moja ya kukijenga chama hicho mkoani humo ambapo alipokelewa na mamia ya wananchi na wapenzi wa chama hicho katika eneo la shule ya tanga katika manispaa ya Songea alipoingia wakati akitokea mkoani Iringa.

Awali baada ya kusikiliza ujumbe toka kikundi cha ngoma cha ya lizombe cha kiwanda cha kukaushia Tumbaku cha Sontop ambacho kimekufa na kilitoa ujumbe uliomuomba kusimamia viongozi wa serikali mkoani humo kuhakikisha kiwanda hicho kinafufuliwa kwa kuwa kilikuwa kikitoa ajira kwa zaidi ya wananchi 2000 ya mkoa huo na kukuza uchumi wa Mkoa wa Ruvuma.

Nape akijibu ujumbe huo alisema kuwa atahakikisha kiwanda hicho kinafufuliwa kwa kuwa amekuja kukagua na kuona kasi ya maendeleo ya miradi waliyoihaidi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 na wanatambuwa kuwa wamepewa dhamana kubwa ya kuhakikisha wananchi wanakuwa na maisha bora .

“ Tutawashugulikia watendaji wabovu wa serikali kwa kuwa kwa utendaji wao mmbovu wanasababisha chama chetu kichukiwe na wananchi kwa hiyo kabla ya kuvuna mabua hatutaki kucheka na nyani “alisema Nauye.

Akizungumza na wanachuo wa chuo kikuu cha mtakatifu Agustino tawi la Songea ambao pia ni wapenzi wa CCM alisema kuwa takwimu zinaonyesha vijana bado wanamapenzi na chama hicho ila wanakwazwa na vita ya kisaikolojia inayoenezwa na vyama vya upinzani kwamba chama hicho kimepoteza mvuto kwao.

Katika kulitambua hilo alisema chama chake kimetenga utaratibu maalum ili kuwajali na kwatambua vijana wake waliovyuoni kwa kutenga Mkoa maalum wenye uongozi kamili ambao utajenga mtandao maalum utakao waunganisha .

Alisema utaratibu huo pamoja na mambo mengine utashughulikia kero zinazowakabili wananfunzi kwa kuwa kunautaratibu wa ovyo umejengeka wa bodi ya mikopo kupeleka fedha za mikopo za wanafunzi baada ya kuandamana kuzidai fedha hizo.

“Chama chetu kinawajari sana vijana na ndio maana wanaonekana wako vizuri kwa kuwa ukitaka kuona maendeleo ya Nchi angalia vijana wake na hivyo katika utaratibu niliousema tutatengeneza kanuni ya kukaa mwaka mmoja madarakani badala ya miaka mitano ili kuwapa nafasi zaidi vijana wetu katika mikoa maalum tunayopanga kutenga kichama.”alisema.

Akitoa dozi kwa vyama vya upinzani kama mwenyewe anavyodai alisema wanoota kupata robo ya hadhi ya CCM wanaota ndoto za mchana na kwamba wameweka mifumo mizuri kwenye chaguzi za chama ili mtu agombee kutokana na uwezo wake kiuongozi na kutokana na uwezo wa fedha zake.

Alisema utaratibu huo unakuja ili kufuta dhana iliyojengeka kwamba chama hicho kiko kwaajiri ya watu wenye fedha na kwamba utaratibu wa chama hicho kuwakumbatia watu wenye fedha ni kukiweka rehani.

Aidha katika ziara yake hiyo ya siku moja ametembelea miradi mbalimbali ya chama ,kuweka jiwe la msingi kwenye maduka ya biashara ya kupangisha ya chama hicho yalijengwa eneo la Mshangano mjini hapa na kuzindua shina la wakeleketwa la mshikamano ambalo amelichangia sh.300,000 na kuwataka wafanyie shughuli za ujasilia mali.

Popular posts from this blog

CATHERINE MASUMBIGANA AWA REDD'S MISS CHANG'OMBE

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

HOTUBA YA MHESHIMIWA PEREIRA AME SILIMA (MB), MWENYEKITI WA BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI (T)