Mamilioni ya Wamisri wakusanyika Cairo katika Medani ya Tahrir

 Mamilioni ya wananchi wa Misri hii leo wameendelea kukukusanyika katika Medani ya Tahrir mjini Cairo baada ya Swala ya Ijumaa, kulalamikia hatua ya Baraza la Kijeshi linaotawala nchini humo ya kung'ang'ania madaraka. Wananchi hao pia wanalalamikia hatua ya wanajeshi hao ya kuchelewesha kutangaza matokeo ya uchaguzi wa rais uliofanyika hivi karibuni. Aidha Wamisri wamelaani kupunguzwa uwezo wa rais wa nchi na uwezekano wa wanajeshi hao kufanya mapinduzi dhidi ya mwenendo mzima wa demokrasia nchini humo.
Hayo yanaripotiwa katika hali ambayo, Baraza la Kijeshi la Misri (SCAF) limesema kwamba litatumia vikosi vya jeshi dhidi ya waandamanaji ambao wamejikusanya katika Medani ya Tahrir kwa madai ya kulinda maslahi ya taifa. Aidha baraza hilo limeikosoa harakati ya Ikhwanul Muslimin eti kwa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa rais mapema na kudai kuwa kutangaza matokeo hayo yasiyo rasmi kumesababisha mgawanyiko na vurugu nchini Misri.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA