MAKAMU WA RAIS DKT. BILALI AZINDUA MAADHIMISHO SIKU YA MAZINGIRA- DUNIANI-KILIMANJARO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti aina ya Mroliondo katika eneo la Chem chem ya Maji Njoro,leo Juni 03, 2012, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika Kitaifa Mkoani Kilimanjaro.
Kwa
muda mrefu sasa, Makamu wa Rais amekuwa mwanamazingira aliye mstari wa
mbele katika usimamizi na uboreshaji wa mazingira na hali ya hewa kwa
ujumla. Amekuwa akishiriki katika ziara mbalimbali za kimazingira na
hali ya hewa ndani na nje ya nchi.