KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA MASHIRIKA YA UMMA YASIFU UTUNZAJI WA KINU CHA NMC IRINGA
Mwenyekiti wa kamati ya bunge hesabu za mashirika ya umma Zitto Kabwe
na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa (CCM ) Lediana Mng'ong'o
ambaye ni mjumbe wa bodi wakipata maelezo ya kinu cha NMC Iringa
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga (CUF) Amina Mwidau akiwa na mbunge wa Mwimbala Mhe.Lugolla
Mwenyekiti wa kamati hiyo Zitto Kabwe (kulia) akipata maelezo ya mitambo mbali mbali katika kinu hicho
Wajumbe wa kamati hiyo wakipata maelezo ya kinu hicho
Hiki ndicho kinu cha NMC Iringa kilivyotunzwa vema
Mjumbe wa kamati hiyo na mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga (CUF) Amina Mwidau (kulia) akiwa na mbunge wa viti malum mkoa wa Iringa Lediana Mng'ong'o ,RAS Iringa Getrude Mpaka , na mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Teresia Mahongo
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga (CUF) Amina Mwidau akiwa na mbunge wa Mwimbala Mhe.Lugolla
Mwenyekiti wa kamati hiyo Zitto Kabwe (kulia) akipata maelezo ya mitambo mbali mbali katika kinu hicho
Wajumbe wa kamati hiyo wakipata maelezo ya kinu hicho
Hiki ndicho kinu cha NMC Iringa kilivyotunzwa vema
Mjumbe wa kamati hiyo na mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga (CUF) Amina Mwidau (kulia) akiwa na mbunge wa viti malum mkoa wa Iringa Lediana Mng'ong'o ,RAS Iringa Getrude Mpaka , na mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Teresia Mahongo
KAMATI
ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma imetembelea mali za kilichokuwa
Kinu cha Kusaga na Kuhifadhi Chakula (NMC) tawi la Iringa na
kujiridhisha kwamba ipo haja ya kumbukumbu zake zote kupitiwa upya huku
ikisifu utunzaji wa kinu hicho na kuahidi kuwaita bungeni viongozi
wa NMC ili kuwapongeza kwa uzalendo wao
Hatua
hiyo imekuja baada ya kuibuka mnong’ong’o kwamba sehemu ya kinu hicho
inafanya kazi kinyemela huku mapato yake yakiwa hayapelekwi hazina.
Pamoja
na tetesi hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo Zitto Kabwe ambaye pia ni
mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo
na badala yake yeye pamoja na wajumbe wa kamati hiyo na wenyeji wao
walijifungia kwa muda ndani ya ofisi, huku wakiwazuia waandishi kusikia
kilichokuwa kikijadiliwa.
Hata
hivyo wakati akitembelea kinu hicho na kuingia katika moja ya majengo
yaliyokuwa yanatumika kwa ajili ya kufunganishia unga kwenye mifuko ya
ujazo tofauti, Kabwe alishangaa kuona lundo la mifuko mipya kwa ajili ya
kufungashia unga uliokuwa ukizalishwa katika kinu hicho.
Mmoja
wa wajumbe wa kamati hiyo alisema kwa sauti ya kunong’ona kwamba kuna
haja ya kujua mapato yaliyokuwa yakikusanywa tangu kinu hicho
kisimamishe uzalishaji wake rasmi yanakwenda wapi.
Tangu
kinu hicho kistishe shughuli zake za uzalishaji kwa zaidi ya miaka
kumi, kumekuwepo na shughuli zingine za watu binafsi zikiendelea hapo,
hata hivyo taarifa ya kilichokusanywa na kinachoendelea kukusanywa
hazikuwa bayana.
Pamoja
na ahadi ya kamati hiyo, Kabwe alitoa mwaliko kwa wafanyakazi kumi wa
iliyokuwa NMC kutembelea bungeni wakati kamati hiyo itakapokuwa
ikiwasilisha taarifa yake kwa kile alichodai wameisadia serikali kulinda
mali za kinu hicho tangu kisimame uzalishaji.
“Wasingekuwa
waaminifu, hii mitambo iliyomo katika kinu hiki na mali zake nyingine
nyingi zingepotea au kuhujumiwa, tunawapongeza na nawalika rasmi
bungeni,” alisema.
Akitoa ahadi hiyo, Kabwe pia alisema mali na mipaka ya kinu hicho itahakikiwa ili uhalali wake uwe bayana.