IDARA ya Habari ( MAELEZO) imetakiwa kujipanga  vizuri ili kuweza kutekeleza majukumu yake ya kuwa Msemaji wa    Serikali ipasavyo; hatua hiyo itasaidia kuepusha malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusiana na utendaji wa Serikali.
Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara wakati akifungua kikao kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali katika ukumbi wa Victoria Palace Jijini Mwanza.
Aidha, Dkt. Mukangara alisema, Idara ya Habari ( MAELEZO) ina jukumu zito la kuwa Msemaji  Mkuu wa Serikali . Hii ni kwa mujibu wa agizo la Serikali Na. C 16 la mwaka  1977.
" Serikali inafanya mambo mengi  mazuri kwa wananchi lakini hayasemwi. Matokeo yake Serikali inaishia kulaumiwa na wananchi bila sababu.
"Ndugu zangu hali hii haikubaliki. Lazima tubadilike na lazima tuseme . Hatuwezi kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali asiyesema." Alisema Dkt. Mukangara.
Dkt. Mukangara aliongeza kuwa Idara ya habari itekeleze jukumu hilo kwa kushirikiana na Wasemaji wa Wizara na Taasisi mbalimbali  za Serikali na Wasemaji hao watambue kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ni Idara ya Habari.
Akizungumzia  kuhusu uhuru wa vyombo vya habari alisema,tunalo tatizo la baadhi ya vyombo vya habari  nchini kudhani kwamba uhuru wa vyombo vya habari hauna mipaka. Hivyo alivitaka vyombo vya  habari vitambue kuwa hakuna nchi yoyote duniani ambayo utendaji wa vyombo vyake vya habri haubna mipaka.
" Wakati wote uhuru wa vyombo vya habari  popote pale huendana na wajibu hata ktika mataifa yaliyoendelea"Alisema Dkt. Mukangara.
Aidha, alivitaka vyombo vya habari kuwa makini katika kutangaza habari zinazohusu mchakato wa mabadiliko ya katiba huku akisissitiza kuonyesha uzalendo wa hali ya juu katika kuwahabarisha wananchi na kutoa elimu.

Popular posts from this blog

CATHERINE MASUMBIGANA AWA REDD'S MISS CHANG'OMBE

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

HOTUBA YA MHESHIMIWA PEREIRA AME SILIMA (MB), MWENYEKITI WA BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI (T)