ASKOFU GAMANYWA

Askofu  Sylvester Gamanywa, Rais wa Wapo Mission International.
Katika toleo lililopita tulianza uchambuzi wa nadharia za kitheolojia ambazo zimekuwa chimbuko la chuki dhidi ya Israeli ndani ya kanisa. Nadharia hizo ni “Theolojia ya Mbadala”, “Theolojia ya Utenganisho” na “Theolojia ya Mabaki”. Kati ya hizi nadharia tatu, inayoongoza kwa chuki dhidi ya Israeli ndani ya kanisa ni ile “Theolojia ya Mbadala”. Hebu tuchunguze kwa ufupi baadhi ya vipengele vinachoashiria kuchochea na kueneza chuki dhid ya Israeli:
Chanzo na madhara
ya thelojia ya mbadala

Nadhari ya Theolojia ya Mbadala ilianza  kati ya karne ya pili na ya tatu tangu kuzaliwia kwa kanisa na ikaanza kujenga mizizi yake yapata muda wa miaka 200 tangu mwanzo wa kanisa. Kilichotangulia ni kuweka kutengeneza “hadharia” kwanza, na baadaye ndipo yakatafutwa maandiko ya kuhalalisha ubaguzi na chuki dhidi ya Israeli.

Baada ya nadhariia hii kuota mizizi katika kanisa la wasio wayahudi, ikajitokeza jeuri, ukaidi na ubinafsi na kujigamba dhidi ya wayahudi na Israeli. Kanisa la wasio wayahudi likashusha thamani na nafasi ya Israeli na kujitoa katika nafasi ya kuitambua na kuiheshimu Israeli

Wakristo wasio wayahudi wengi wakawa wanajivunia kuwa wafuasi wa Agano Jipya kama ilivyokuwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume. Lakini pamoja na majivuno haya bado wakasahau kwamba, maandiko yaliyotumika katika kanisa la Matendo bado yalikuwa ni maandiko ya Kiebrania, ya Agano la Kale mpaka kwenye karne ya nne ambapo Maandiko ya Agano Jipya yalikusanywa na kutambuliwa rasmi

Hata baada ya Agano Jipya kutambuliwa rasmi, ndani yake bado Israeli imetajwa kiasi kwamba, pasipo nafasi ya Israeli na wayahudi hivi leo, huwezi kutafsiri nabii za kibiblia, hususan nabii zile zinazoendelea kutimia ndani ya nchi hiyo kwa hivi sasa Aidha, Maandiko mengi katika Agano Jipya hupoteza maana yake halisi pale inapodaiwa kuwa  wayahudi nafasi yao imechukuliwa na kanisa

Mpaka hivi sasa kutokuitambua Israeli kunayafanya maandiko ya kiebrania ya a Agano la Kale kupoteza uzito na maana yake kwa matumizi ya sasa; Ikiwa ni pamoja na kupoteza fursa ya kushiriki katika mpango wa Mungu na unabii kwa ajili ya Kanisa, Israeli na ulimwengu wa leo

Kanisa kutokuamini kutimia kwa
unabii kuhusu urejeo wa Israeli

Nadharia ya theolojia ya Mbadala iliota mizizi ndani ya kanisa tangu karne ya pili. Pamoja na kwamba ziko nabii ndani ya maandiko katika Biblia zilizotabiri urejesho wa Israeli kutoka kwenye mataifa lilipotawanyikia, kanisa halikuamini kwamba kutumia kwa unabii huo kutafanyika kablal ya ujio wa Kristo mara ya pili duniani.

Changamoto dhidi ya nadhari ya Mbadala ilianza rasmi baada ya Israeli kurejea katika nchi yao, na kuanza kuumiliki mji wa Yerusalemu kama zamani za historia yake. Urejeo huu wa Israeli uliifanya theolojia ya Mbadala kupoteza maana yake, na ndipo hila za kibaguzi za miaka mingi dhidi ya Israeli zilipoanza kuwa dhahiri.

Kuanzia wakati huo, baadhi ya viongozi wa makanisa wakaanza kurejea katika maandiko na kuchunguza nabii zilizotabiriwa kuhusu Israeli na kugundua kwamba urejeo wa Israeli ni kutumia kwa baadhi ya nabii hizo. Ndipo zilipoanza juhudi za makusudi za kulitaka kanisa kutubia dhambi ya kukumbatia nadharia potofu na za kibaguzi dhidi ya Israeli.



Kwako msomaji mpenzi, niseme waziwazi pasipo kumung’unya maneno hapa. Amini usiamini, kubali usikubali, ukweli uko dhahiri katika macho ya ulimwengu kwamba, uwepo wa Israeli pale Mashariki ya Kati, ni utumilifu wa nabii zilizotangulia kutolewa juu ya Israeli. Wakati ulimwmengu wa kisiasa na kidiplomasia unadai kuwa ni “uvamizi na kukalia kwa mabavu” maeneo yale; kinabii kwa mujibu wa Biblia, huko ni “kurejeshewa na Mungu ardhi yao waliyopewa na Mungu kama wenye hatimiliki ya kudumu”. Najua  hii inweza kuudhi au kukera sana, lakini ndio ukweli wenyewe ambao unapaswa kusemwa na kutetewa na kila Mkristo mwenye imani halisi katika Biblia takatifu.

“Ukawaambie, Bwana MUNGU asema hivi; tazama nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe; nami nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo, juu ya milima ya Israeli; na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote; wala hawatakuwa mataifa mawili, wala hawatagawanyika kuwa falme mbili tena, hata milele.” (Eze.37:21-22)

Kwa mujibu wa maandiko haya ya kinabii, hivi sasa tunashuhudia kwamba, Israeli ni taifa huru na taifa moja na kiongozi mmoja. Hakuna mgawanyiko wa kitaifa kama ilivyokuwa pale waliposambaratishwa na kutawanywa ulimwengu mzima. Ni muhimu kuzingatia maneno yasemayo: “…..name nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe…”

Pengine msomaji unaweza kujiuliza ni kwanini Mungu aliamua kuwarejesha tena? Jibu ni moja tu. Mungu akisema neno lake halitanguki. Lazima atalitimiza. Na hasa anpokuwa amesema katika mfumo wa ahadi. Pamoja na kwamba Israeli waliendelea kumwasi Mungu kwa njia zote, ahadi za Mungu kwa Ibrahimu ziliwekewa kinga ya ulinzi mpaka zitimie. Unaweza kusoma maandiko hapa chini ili kuona uzito wa maneno yalimo ndani yake:

“BWANA asema hivi, awapaye watu jua, ili kuuwa nuru wakati wa mchana, na amri za mwezi na nyota, ili kuwa nuru wakati wa usiku, aichafuaye bahari, hata mawimbi yake kuvuma; BWANA wa Majeshi, ndilo jina lake; amri hizi, zikiondoka, zisiwe mbele zangu, asema BWANA, ndipo na wazao wa Israeli nao wataacha kuwa taifa mbele zangu milele.” (Yer.31:35-36)

Unaweza kuoa jinsi Mungu alivyojifunga mwenyewe kwa maneno ya mazito kuhusu uwepo wa taifa la Israeli kama nchi kamili na taifa teule.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA