AHADI KUTOKA CCM

CHAMA cha Mapinduzi, kimesema ahadi ilizozitowa kwa wananchi katika kuinadi Ilani ya chama hicho inazitekeleza kwa hatua ili kuwaletea wananchi maendeleo katika maeneo yao.
Aidha chama hicho, kimesema kinakusudia hadi kufikia mwaka 2015 iwe tayari yake ya Uchaguzi wa mwaka 2010-2015 za kuwaletea Maendeleo, zipo pale pale na itaendelea kufanya hivyo na kuhakikisha kuwa kero mbali mbali zinapatiwa ufumbuzi mapema iwezekanavyo kabla ya 2015 hatuwa kwa hatuwa.
Akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Mkanyageni Pemba, Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM, na Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia , Profesa, Makame Mnyaa Mbarawa, wakati wa kukabidhi mashine ya kusukumia maji kwa wananchi wa Jimbo hilo, alisema kuwa CCM, ina kila sababu ya kufanya hivyo kwa kuwa ndicho chama kinachoiongoza nchi.
Alisema huduma nyingi za kijamii ikiwemo, barabara, maji safi na salama, afya, miradi ya elimu imeweza kutekelezwa kwa kupitia ilani ya chama hicho cha kuwaletea maendeleo wananchi wake.
Mjumbe huyo wa Kamati kuu ya CCM Taifa, alisema CCM, haijakata tamaa ya kutotekeleza ahadi zilizobaki ikiwa ni kuwaenzi wapiga kura wa Jimbo hilo na hata waliokuwa hawakupiga kura.
“ Tuna kila sababu ya kuwaleteeni Maendeleo katika Jimbo hili kwa kadri inavyowezekana hatuwa bada hatuwa kwa vile sisi ni wananchi wa Jimbo hili na maendeleo ya hapa yataletwa na sisi wenyewe hatokei mwengine akatuletea “ alieleza Profesa Mnyaa.
Aliendelea kusema kuwa CCM, ipo kwa ajili ya watu na ipo kwa ajili ya maendeleo , hivyo aliwataka Viongozi wengine kushirikiana na wale wenyenia ya kuletea maendeleo kwa Wananchi kwa vile Ustawi wa Wananchi ni kuwepo maendeleo katika sehemu zao wanazoishi.
Mnyaa, alieleza kuwa kila Mwananchi wa Jimbo hilo watahakikisha kuwa anafikiwa na maendeleo mbali mbali katika mahala alipo yakiwemo Maji, Afya , Elimu , Barabara n.k kwa vile ni wajibu wao kama viongozi.
"Sisi hatuna tatizo wala hatua nongwa kwa vile Wananchi wa Jimbo hili nawakuwa na kura nyingi , lakini tutahakikisha kuwa Mkanyageni inakuwa na maendeleo ya kutosha,”alisema.
Hata hivyo, aliwataka Vijana wa Jimbo hilo kuwa wabunifu wa maendeleo ili kuisaidia Serikali katika harakati zake za kuwaletea wananchi maendeleo kwa kujitokeza katika kazi mbali mbali za ujenzi wa taifa.
Nae Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Meja mstaafu, Juma Kassim Tindwa, alimpongeza mjumbe huyo wa Kamati kuu ya CCM, kwa juhudi zake za kuleta maendeleo kwa wananchi wa Jimbo hilo, na kuwataka wananchi hao kuyalinda na kuyathamini maendeleo hayo.
“ Ni vyema wananchi wa Jimbo la Mkanyageni, mukaona kuwa maendeleo yaliopo katika jimbo lenu ni yenu wenyewe , kwa maana hiyo muyalinde na musikubali kuja mtu kuyaharibu” alisema Tindwa.
Kwa upande wake, Afisa mdhamini wa nWizara ya Ardhi , Makaazi , Maji na Nishati Pemba, Hemed Salim, aliwahakikishia wananchi wa Jimbo hilo kufaidika na huduma hiyo ndani ya wiki moja kuanzia sasa kwa kuwa vifaa vyote vimekamilika na vimeshakabidhiwa .
Mashine hiyo ya Maji aliyoikabidhi Profesa Mnyaa kwa wananchi ina thamani ya shilingi milioni 19 na ina uwezo wa kufanya kazi kwa muda wa miaka 20.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA