Mkuu Wa Jeshi la Polisi Nchini Saidi Mwema
............................................................

JESHI la Polisi nchini limeingia katika kashfa nyingine baada ya kijana Charles Patrick Paulo mkazi wa kijiji cha Mundemu wilayani Bahi mkoani Dodoma kulishushia tuhuma nzito za kupora fedha na kumbambikia kesi ya unyang’anyi.

Kesi hiyo iliyoendeshwa kasi ilimtupa jela miaka 15 kabla ya kuachiwa huru miezi sita baadaye baada ya kushinda rufaa.

Julai 20 mwaka jana, Paulo alitiwa hatiani na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mundemu F. Bulyota kwa shitaka la unyang’anyi kifungu namba 286 K/A Sura 16 na kutupwa jela kwa miaka 15.

Hukumu hiyo ilianzisha safari mpya ya maisha kwa kijana Paulo ambaye aliachana na maisha ya uraiani akimuacha mchumba wake, Upendo Masila akiwa na ujauzito wa miezi miwili huku
yeye akipelekwa katika Magereza ya Isanga kuanza kutumikia kifungo chake.

Lakini kwa vile alijua kuwa hukumu yake imetokana na uonevu wa Polisi, wiki moja baadaye kijana Paulo aliwasilisha rufani yake kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma akipinga hukumu hiyo, rufani ambayo ilizaa matunda Januari 26 mwaka huu, pale Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Dodoma, R.M Ngimilanga alipotoa hati ikiamuru
kijana huyo kuachiwa huru mara moja.

“Siku ya tarehe 20/07/2011 – Charles S/O Patrick Paulo Mshitakiwa

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA