CCM KUKATA RUFANI DHIDI YA HUKUMU YA KESI UCHAGUZI IGUNGA
Taarifa
iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM, Itikadi na Uenezi,
Nape Nnauye mchana leo, imeseme kufuatia kutoridhishwa na hukumu
iliyotolewa jana na Jaji wa Mahakama hiyo, Mary Shangali, kitakata
rufani.
"Chama
Cha Mapinduzi kimetafakari hukumu ya kesi ya uchaguzi iliyotolewa jana
Agosti 21, 2012 na Mahakama Kuu kanda ya Tabora. Kimejiridhisha na
kufanya uamuzi wa kukata rufaa dhidi ya hukumu ya kesi ya uchaguzi,
dhidi ya Mbunge wa jimbo la Igunga mkoani Tabora Dokta Dalali Peter
Kafumu.Kusudio hilo linatokana na kutorishwa na hukumu hiyo". imesema
taarifa hiyo.
Jana
Jaji Mary Shangali katika hukumu yake, alisema ametengua ushindi wa
Dk. Kafumu baada ya kurishishwa na madai saba kati ya 17
yaliyowasilishwa katika mahakama hiyo na Mlalamilikaji, aliyekuwa
mgombea kwa tiketi ya Chadema, Joseph Kashindye.