JUMLA YA BILIONI 148 HUPOTEA NDANI YA BARA LA AFRIKA

Ashura Mohamed wa Fullshangwe-ARUSHA
JUMLA ya  kiasi cha dola za Kimarekani Bilion 148   huwa zinapotea
ndani ya Nchi za bara la Afrika kila mwaka kutokana na kuwepo kwa
mianya mingi ya rushwa  na badala yake fedha hizo zinapelekwa katika
nchi za Ugaibuni hali ambayo inasababisha madhara makubwa sana kwa
nchi ya A frika


Hayo yameelezwa na mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana
na Rushwa (TAKUKURU)Dkt Edward hosea wakati akizungumza katika mkutano
wa bodi ya ushauri wa masuala ya Rushwa kwa nchi za bara la Afrika
jijini hapa


Aidha dkt Hosea alisema kuwa kiwango hicho cha fedha hupotea kutokana
na baadhi ya mianya ya Rushwa ambayo imo kwenye nchi hizo na badala
yake fedha hizo zinapelekwa kwenye nchi za Ugaibuni


Alifafanua kuwa kutokana na hali hiyo ya upotevu wa fedha hizo
unachangia kwa kiwango kikubwa sana hata kukithiri kwa rushwa ndani ya
Nchi hizo hali ambayo nayo inachangia hata maendeleo duni ya nchi hizo
za bara la Afrika

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA