HASHEEM THABEET KUJENGA UWANJA WA KISASA WA MPIRA WA KIKAPU


Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Kumbukumbu ya Lord Baden Powell, Kanali Idd Kipingu akizungumza machache mbele ya wageni wake waliofika mapema leo shuleni hapo kwa ajili ya kuangalia namna ya kujenga uwanja wa mchezo wa mpira wa kikapu.
Mchezaji wa Kimataifa wa Tanzania, anayechezea timu ya Portland Trail Blazers ya Marekani kwenye Ligi ya NBA, Hasheem Thabeet akizungumza jambo mbele ya wanafunzi wa shule ya sekondari  ya Lord Baden Powell Memorial High School,wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa kiwanja cha mpira wa kikapu shuleni hapo mapema leo Bagamoyo,nje kidogo ya jiji la Dar,kulia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la mpira wa kikapu Tanzania, Phares Magesa.Hasheem Thabeet ameahidi kuwajengea uwanja wa mpira wa kikapu shuleni hapo. 

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA