Asamoah na Dede Ayew nje


Mshambulizi matata Asamoah Gyan hayuko kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ghana kilichotajwa na Kocha Kwesi Appia.
Asamoah Gyana na Dede Ayew wote nje
Gyan ameachwa nje hata baada ya shinikizo kwamba ajumuishwe kwenye kikosi cha Ghana.

Wengine waliotemwa ni mwamba wa Chelsea Michael Essien na Andre 'Dede' Ayew ambaye ana jeraha.
John Paintsil na aliyekuwa nahodha wa Ghana John Mensah nao pia hawamo.

katiuka kikosi chake kipya kocha Appiah amewajumuisha wachezaji sita wapya wengi wakiwa wanachezea soka la kulipwa ulaya. hata hivyo amejumuisha wachezaji tisa toka ligi ya nyumbani.

Asamoah Gyan aliamua kujiondoa toka timu ya taifa baada ya kushambuliwa na mashabiki baada ya uchezaji wake duni katika michuano ya kombe la bara afrika la hivi majuzi.

ilikuwa inatarajiwa kwamba angelirejea katika timu kabla ya mwezi ya Juni.

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa

MATAJIRI WATANO WANAOONGOZA TANZANIA