MAJAMBAZI YAPORA RAIA WA UHOLANZI
Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma linawasaka Watu wawili kwa tuhuma za Unyang’anyi wa kutumia nguvu baada ya kuwatisha kwa jambia wasichana wawili raia wa Uholanzi na kisha kuwapora vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni moja laki mbili na sitini na nne elfu. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Bw. ZELOTHE STEPHEN alisema Tukio hilo lilitokea muda wa saa saba na dakika arobaini na tano mchana katika eneo la area D Wilaya ya Dodoma Mjini, Karibu na nyumba inayojengwa kwa ajili ya 0fisi na Makazi ya Mh. Waziri Mkuu Bw. MIZENGO KAYANDA PETER PINDA. Alitaja vitu vilivyoporwa katiika tukio hilo kuwa ni Kamera ya digitali aina ya Canon, Simu mbili za mkononi aina ya Nokia na Samsung, Begi la Mgongoni, Viatu vya wazi pea mbili (Sandal) Taulo la Hostel, Sketi, Wallet na Pesa za kitanzania shilingi 40,000/=. Aidha aliwataja Waathirika wa Unyang’anyi huo kuwa ni wa LISA D/O LEMEN mwenye umri wa ...