SIMBA KUMCHUKUA SHEDRACK NSAJIGWA


Siku chache baada ya mchezaji Shedrack Nsajigwa kumaliza mkataba wa kuichezea klabu ya Yanga huku akiripotiwa kuwepo nchini Kenya akifanya mazungumzo na klabu ya Gor Mahia, leo taarifa za uhakika kutoka kwenye kamati ya usajili ya Simba, zinasema viongozi wa mabingwa wa Tanzania wapo tayari kumsaini nahodha huyo wa zamani wa Yanga na Taifa Stars.

Simba ambao leo hii wamepata pigo baada ya beki wao wa upande wa kulia Said Nassoro Chollo kuripotiwa kupata majeraha makubwa kama yale yaliyompata Uhuru Seleman, wanamuona Nsajigwa kama mbadala halisi atakayefaa kuziba mapengo kwenye safu ya ulinzi ya timu hiyo.

Mtoa taarifa anasema, "Nsajigwa bado ni mchezaji mzuri sana, na uwezo mkubwa na kikubwa zaidi ni uzoefu alionao ambao ni hazina kubwa kwa klabu kama yetu ambayo sasa tunajaribu kuingiza vijana wadogo kama akina Singano, na ndio maana tumeamua kuanza harakati za kumsajili na kwa hakika tutafanikiwa."

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

CATHERINE MASUMBIGANA AWA REDD'S MISS CHANG'OMBE

HOTUBA YA MHESHIMIWA PEREIRA AME SILIMA (MB), MWENYEKITI WA BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI (T)