WAKULIMA WA TUMBAKU WAHIMIZWA KUSHIRIKI SENSA
Wakulima wa Tumbaku wilayani Singida, wamekumbushwa kujitokeza kushiriki sensa ya watu na makazi itakayofanyika Agost 26, mwaka huu. Wito huo ulitolewa na Mkuu wa wilaya hiyo, Fatma Toufiq, alipozungumza na wakulima pamoja na wakazi wa kijiji cha Mitundu. Alisema sensa hiyo inalenga kupata idadi ya watu waliopo ili kufahamu shughuli za kiuchumi, kielimu na kiundombinu kwa lengo la kupanga maendeleo ya nchi na watu wake. “Sensa ni muhimu na inawezesha kufahamu idadi ya watu katika maeneo yetu ili kufahamu shughuli zao za kiuchumi, kielimu na miundombinu ili tupannge maendeleo” alisema Toufiq. Toufiq alitumia fursa hiyo kuwaasa wananchi wilayani Singida, kujitokeza kwa wingi pindi muda utakapofika ili kila mmoja ahesabiwe kwa faida yake na taifa. Mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika cha Wakulima wa tumbaku (CETCU), kanda ya kati Yassin Dagaki, akitoa taarifa ya maendeleo ya kilimo cha zao hilo , alisema msimu wa mwaka 2009/2010 uzalishaji uliongezeka kwa...