MAKAMU Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula:“Kwa kuwa tayari Rais ameshasema kuwa suala la gesi kubaki Kusini halikubaliki, wanaompinga ni waasi,”



MAKAMU Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula
---
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula amesema viongozi wanaopinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam wanafanya uasi na kuvunja nidhamu ya demokrasia.Mangula alitoa kauli hiyo jana alipokuwa anazungumzia kauli za makada wa CCM wanaompinga Rais Jakaya Kikwete kuhusu msimamo huo wa Serikali.
“Kwa kuwa tayari Rais ameshasema kuwa suala la gesi  kubaki Kusini halikubaliki, wanaompinga ni waasi,” alisema.
Ingawa Mangula hakuwataja makada hao, Mwenyekiti wa CCM Manispaa ya Mikindani mkoani Mtwara, Ali Chinkawene na Mbunge wa Mtwara Mjini, Hasnain Murji ni miongoni mwa makada waliopinga suala hilo waziwazi.

Chinkawene alisema msimamo wa CCM Mkoa wa Mtwara, ni kuungana na wananchi kupinga gesi kusafirishwa kwenda Dar es Salaam na kwamba Serikali inapaswa kujenga mitambo ya kuzalisha umeme mkoani Mtwara.
Mbunge Murji alikwenda mbali zaidi akisema yupo tayari ikibidi, kuvuliwa ubunge kwa kutetea masilahi ya Wanamtwara kuliko kuona gesi hiyo ikisafirishwa kwenda Dar es Salaam.Mangula alisema mtu mmojammoja, hawezi kutoa msimamo wake na kudai kuwa ni msimamo wa chama.Kwa habari zaidi Bofya na Endelea.........>>>>>>

Popular posts from this blog

MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO

CATHERINE MASUMBIGANA AWA REDD'S MISS CHANG'OMBE

HOTUBA YA MHESHIMIWA PEREIRA AME SILIMA (MB), MWENYEKITI WA BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI (T)