Umoja blog ni blog ya kijamii,siasa,burudani na michezo
MKUTANO WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO TASWA WAFANYIKA BAGAMOYO LEO
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Mwenyekiti
wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys Bw.
Ridhiwan Kikwete akifungua mkutano mkuu wa chama cha waandishi wa
habari za michezo TASWA unaofanyika kwenye Hoteli ya Kiromo View
Bagamoyo mkoani Pwani ambao unajadili mambo mbalimbali ya Maendeleo na
changamoto zinazokabili chama hicho.
Waanishi wa habari za michezo ambao ni wanachama kutoka vyombo mbalimbali nchini wanahudhuria mkutano huo ambao ni wa siku moja.
Mwenyekiti
wa Chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA Bw. Juma Pinto
akimkaribisha mgeni rasmi ili kufungua mkutano huo leo asubuhi
unaofanyika kwenye hoteli ya Kiromo View Bagamoyo.
Katibu
wa Chama cha Waandishi wa habari za michezo TASWA Bw. Amir Mhando
akizungumza katika mkutano huo, kutoka kulia ni Makamu Mwenyekiti wa
TASWA Maulid Kitenge, Mwenyekiti Juma Pinto, Mgeni rasmi Ridhiwan
Kikwete na kushoto ni George John Katibu Msaidizi.
Mtaalam
wa SACCOS kutoka Manispaa ya Ilala Bw. Luambano akitoa mada kuweka na
kukopa kwa waandishi wa habari wanachama wa TASWA waliohudhuria katika
mkutano huo
Kutoka
kulia ni waandishi wakongwe Mwina Kaduguda, Mzee Wlly Chiwango na Mzee
Salim Said Salim kutoka Zanzibar wakiwa katika mkutano huo.
Kutoka kulia ni Shafii Dauda, Erasto na Ibrahim Masoud wakiwa katika mkutano huo.
Kutoka kulia ni Elizaberth Mayemba , Timzo Kalugira na Crala Alphonce wakifuatilia mada katika mkutano huo.
Kutoka kushoto ni Elius Kambili, Alfred Lucas na Salum Jaba wajumbe wa kamati ya utendaji ya TASWA wakiwa katika mkutano huo.
Kutoka kulia ni Mgaya Kingoba, Salum Jaba, Richard Mwaikenda na Tulo Chambo wakifuatilia mada katika mkutano huo.
Wajumbe
mbalimbali wakihudhuria mkutano wa Chama cha Waandishi wa habari za
michezo TASWA kwenye hoteli ya Kiromo View mjini nje kidogo ya mji wa
Bagamoyo mkoani Pwani .
Mara nyingi wengi wetu tumekuwa katika mahusiano na wapenzi wetu lakini hali sio kama ile ya awali wakati mnaanza mapenzi yenu. Wanawake wengi wanalalamika kuwa hawaoni upendo ule waliouzoea zamani wakati mapenzi yanaanza. Hata wanaume wengine wanalalamika pia kuwa penzi limeteremka kiwango baina yao . Mara zote hushuka huku kwa ukaribu (intimacy) hakupangiliwi au kutazamiwa bali huja taratibu pasipo wapenzi kutambua, mara lugha hubadilika, muda wakuwa pamoja hupungua, mambo huanza kufanywa kwa mazoea, vilivyo zoeleka kufanyika havionekani tena na taratibu hali hii ikikomaa huathiri hata tendo la ndoa. Katika hatua hii, wapenzi huanza kuchokana na kutotamaniana, hapa ndio kwenye upenyo wa mmoja au wote kuwaza njia mbadala. Wengi walioachana au kutalikiana nao walipitia njia hii pia. Ili kuepuka yote haya, haunabudi kujifunza njia za kuwasha moto wa upendo kila wakati na kuongeza ukaribu (intimacy) kati yenu. Njia za kukusaidia 1. ...
Redds Miss Chang’ombe 2012, Catherine Masumbigana 21, (katikati) akipunga mkono mara baada ya kusimikwa rasmi kuwa mshindi wa taji hilo. Kulia ni mmshindi wa pili, Jesca Haule (18) na Mshindi wa tatu Zulfa Bundala. Masumbigana aliwashinda warembo wengine 13 katika shindano hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Quality Center jijini Dar es Salaam Juni 10, 2012. Tano bora ya Miss Chang’ombe 2012 ambao wote wamepata tiketi ya kushiriki shindano la Miss Temeke 2012 wakiwa katika picha ya pamoja. Kutoka Kushoto ni Zulfa Bundala (21), Jesca Haule (18), Catherine Masumbigana (21), Miriam Nkisigwa (20) na Flora Kazungu. Warembo wakicheza show maalum ya ufunguzi Vazi la ufukwenu, Kutoka kulia ni Restituta Faustiney, Wensley Mabula na Clara Diu. Warembo Flora Mayasa (kulia) Catherine Masumbigana (katikati) na Elizabeth Mushi wakiwinda point na vazi la ufukweni. Mkali wa Bongo Fleva Nassib Abdul 'Diamond' na vija...
HOTUBA YA MHESHIMIWA PEREIRA AME SILIMA (MB), MWENYEKITI WA BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI (T) KWENYE UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA WIKI YA NENDA KWAUSALAMA BARABARANI KITAIFA MKOANI IRINGA TAREHE 17 SEPTEMBA, 2012 Mhe. Mgeni Rasmi Mhe. Eng. Gerson Hosea Lwenge (Mb), Naibu Waziri wa Ujenzi na Makamo Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Ndugu Mbarak Abdulwakil, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Ndugu Herbert Mrango, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb), Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ndugu Said Ally Mwema, Inspekta Jenerali wa Polisi Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Iringa Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani (T) Wageni Waalikwa Wanahabari Mabibi na Mabwana Asalaam Aleikum, Amani ya Mungu iwe juu yenu Awali ya yote napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwako Mhe. Mgeni rasmi kwa kukubali kwako kuungana nasi katika ufunguzi wa wiki ya maadhimisho...