Said Bahanuzi ni mshambuliaji mahiri wa timu ya Yanga ya nchini Tanzania jana alithibitisha kwamba yeye ni mchezaji halali wa Yanga na ataendelea kuwa mchezaji wa Yanga kwa muda wa miaka miwili kwa tamko hilo Bahanuzi ameondoa utata uliokuwa unaanza kuvuma jijini Dar Es Salaam na nchi kwa ujumla kwamba huenda mchezaji huyo amehamia timu pinzani ya Simba ambao haikufanya vizuri katika mashindano ya hivi karibuni ya Kagame Cup iliyoshirikisha timu mbali mbali za klabu za afrika mashariki na kati na ikiwemo kuiwakilisha timu ngeni ya kutoka Congo ya Vita FC ingawa timu hiyo ilishika nafasi ya tatu kwenye michuano hiyo.
CATHERINE MASUMBIGANA AWA REDD'S MISS CHANG'OMBE
Redds Miss Chang’ombe 2012, Catherine Masumbigana 21, (katikati) akipunga mkono mara baada ya kusimikwa rasmi kuwa mshindi wa taji hilo. Kulia ni mmshindi wa pili, Jesca Haule (18) na Mshindi wa tatu Zulfa Bundala. Masumbigana aliwashinda warembo wengine 13 katika shindano hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Quality Center jijini Dar es Salaam Juni 10, 2012. Tano bora ya Miss Chang’ombe 2012 ambao wote wamepata tiketi ya kushiriki shindano la Miss Temeke 2012 wakiwa katika picha ya pamoja. Kutoka Kushoto ni Zulfa Bundala (21), Jesca Haule (18), Catherine Masumbigana (21), Miriam Nkisigwa (20) na Flora Kazungu. Warembo wakicheza show maalum ya ufunguzi Vazi la ufukwenu, Kutoka kulia ni Restituta Faustiney, Wensley Mabula na Clara Diu. Warembo Flora Mayasa (kulia) Catherine Masumbigana (katikati) na Elizabeth Mushi wakiwinda point na vazi la ufukweni. Mkali wa Bongo Fleva Nassib Abdul 'Diamond' na vija...
