Said Bahanuzi ni mshambuliaji mahiri wa timu ya Yanga ya nchini Tanzania jana alithibitisha kwamba yeye ni mchezaji halali wa Yanga na ataendelea kuwa mchezaji wa Yanga kwa muda wa miaka miwili kwa tamko hilo Bahanuzi ameondoa utata uliokuwa unaanza kuvuma jijini Dar Es Salaam na nchi kwa ujumla kwamba huenda mchezaji huyo amehamia timu pinzani ya Simba ambao haikufanya vizuri katika mashindano ya hivi karibuni ya Kagame Cup iliyoshirikisha timu mbali mbali za klabu za afrika mashariki na kati na ikiwemo kuiwakilisha timu ngeni ya kutoka Congo ya Vita FC ingawa timu hiyo ilishika nafasi ya tatu kwenye michuano hiyo.
MAMBO 6 YA KUZINGATIA KATIKA MAHUSIANO
Mara nyingi wengi wetu tumekuwa katika mahusiano na wapenzi wetu lakini hali sio kama ile ya awali wakati mnaanza mapenzi yenu. Wanawake wengi wanalalamika kuwa hawaoni upendo ule waliouzoea zamani wakati mapenzi yanaanza. Hata wanaume wengine wanalalamika pia kuwa penzi limeteremka kiwango baina yao . Mara zote hushuka huku kwa ukaribu (intimacy) hakupangiliwi au kutazamiwa bali huja taratibu pasipo wapenzi kutambua, mara lugha hubadilika, muda wakuwa pamoja hupungua, mambo huanza kufanywa kwa mazoea, vilivyo zoeleka kufanyika havionekani tena na taratibu hali hii ikikomaa huathiri hata tendo la ndoa. Katika hatua hii, wapenzi huanza kuchokana na kutotamaniana, hapa ndio kwenye upenyo wa mmoja au wote kuwaza njia mbadala. Wengi walioachana au kutalikiana nao walipitia njia hii pia. Ili kuepuka yote haya, haunabudi kujifunza njia za kuwasha moto wa upendo kila wakati na kuongeza ukaribu (intimacy) kati yenu. Njia za kukusaidia 1. ...