Mamilioni ya Wamisri wakusanyika Cairo katika Medani ya Tahrir
Hayo yanaripotiwa katika hali ambayo, Baraza la Kijeshi la Misri (SCAF) limesema kwamba litatumia vikosi vya jeshi dhidi ya waandamanaji ambao wamejikusanya katika Medani ya Tahrir kwa madai ya kulinda maslahi ya taifa. Aidha baraza hilo limeikosoa harakati ya Ikhwanul Muslimin eti kwa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa rais mapema na kudai kuwa kutangaza matokeo hayo yasiyo rasmi kumesababisha mgawanyiko na vurugu nchini Misri.