Maharamia wateka meli ya Italia
Jeshi la wanamaji la Italia limesema maharamia wamekwea na kuchukua udhibiti wa meli ya mafuta ya Italia katika bahari ya Hindi.
Meli ya Ujerumani ambayo pia imetekwa
Msemaji wa jeshi la wananamaji amesema hakuna aliyejeruhiwa miongoni mwa mabaharia 17 kutoka India na wataliano watano.
Maharama wamejipatia mamilioni ya dola
Meli hiyo imebeba shehena ya mafuta yaliyokuwa yakipelekwa katika bandari ya Pasir Gudang nchini Malaysia, limeripoti shirika la habari la Reuters.
Wanajeshi wa Marekani wakiwa na maharamia
Umoja wa Ulaya umesema meli hiyo imetekwa na mashua moja ikiwa na maharamia watano.
Maharamia wa Somalia
Maharamia wa Kisomali wametjipatia mamilioni ya dola katika miaka ya hivi karibuni kwa kuteka meli za mizigo katika njia inayotumiwa na meli katika pembe ya Afrika.