TFF IKO MBIONI KUJIUNGA NA SUPER SPORT
SHIRIKISHO la Soka
Tanzania, TFF, liko katika mchakato wa mazungumzo na kituo cha
SuperSport cha Afrika Kusini kwa ajili ya kuonyesha mechi zake za Ligi
Kuu msimu ujao.
Wakati TFF ikijipanga kufanya hivyo, kituo hicho tayari kinafanya hivyo kwa Ligi Kuu ya Kenya na Uganda.
Itakumbukwa, Super Sport ilikuwa ikionyesha baadhi ya mechi za Ligi Kuu Bara na zaidi ni zile zinazohusisha timu za Simba na Yanga na kuonekana sehemu mbalimbali duniani.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Walas Karia alisema katika mazungumzo ya kwanza pande hizo mbili zilishindwa kufikia makubaliano na baada ya Super Sport kutoa kupendekeza yake kuwa baadhi ya mambo lazima yafanyike iweze kudhamini ligi hiyo.
"Kwa sasa kamati ipo katika harakati kukutana na viongozi wa Super Sport kuhakikisha Ligi Kuu msimu ujao inakuwa ya kuvutia ikiwemo pia kutafuta wadhamini mbalimbali lengo likiwa kupunguza makali ya gharama za uendeshaji kwa klabu."
Wakati TFF ikijipanga kufanya hivyo, kituo hicho tayari kinafanya hivyo kwa Ligi Kuu ya Kenya na Uganda.
Itakumbukwa, Super Sport ilikuwa ikionyesha baadhi ya mechi za Ligi Kuu Bara na zaidi ni zile zinazohusisha timu za Simba na Yanga na kuonekana sehemu mbalimbali duniani.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Walas Karia alisema katika mazungumzo ya kwanza pande hizo mbili zilishindwa kufikia makubaliano na baada ya Super Sport kutoa kupendekeza yake kuwa baadhi ya mambo lazima yafanyike iweze kudhamini ligi hiyo.
"Kwa sasa kamati ipo katika harakati kukutana na viongozi wa Super Sport kuhakikisha Ligi Kuu msimu ujao inakuwa ya kuvutia ikiwemo pia kutafuta wadhamini mbalimbali lengo likiwa kupunguza makali ya gharama za uendeshaji kwa klabu."